Jumamosi, 24 Julai 2021
Jumanne, 28 Januari 2020
Nioneshe Marafiki Zako nami Nitakuonesha Maisha yako ya Baadaye!
Jumatano, 24 Aprili 2019
Soko Huru na Faida Zake.
Katika hali ya kawaida na inayouchochea uchumi wa eneo lolote ni kuacha bei ya bidhaa ipangwe na soko lenyewe.
Soko linapangaje bei!?
Kwanza mzalishaji huzalisha akitegemea kuuza kwa faida yaani gharama zote za uzalishaji zirejeshwe na ziada. Ukianza kuuza mazao yako pale utakapoona uhitaji wa bidhaa zako ni mkubwa sana ndipo unaongeza uzalishaji ili kuwafanya wateja wako wapate bidhaa yako pasipo shida. Na katika kuongeza uzalishaji pia unaweza kuongeza bei ili kupunguza wateja wasiolazima ili ujue vyema idadi ya wateja wako na ujipange kuzalisha kile kitakachowakidhi wateja hao.
Soko huru husaidia suala la kupunguza bei na au kuongeza bei kuwa chini ya muuzaji na mnunuaji pekee.
Jumapili, 15 Julai 2018
Jee dhamira yako ya mafanikio ni hai!?
Lakini cha kushangaza utaona siku, wiki, mwezi na mwaka unapita lakini hakuna kitu kimefanyika waingereza wanasema "no tangible development seen" hakuna maendeleo yanayoonekana.
Nini tatizo!? Ni muhimu kufahamu bila ya kuwa na moyo wa kujikana na kudhamiria kufikia mipango na malengo yako hakika ndoto na mipango yako itaendelea kuwa ndoto bila kufikia uhalisia wowote.
Jambo lolote ukilipanga na kudhamiria kulifikia nikutie moyo, inawezekana kabisa kwani hata Mungu muumbaji wetu anafanya kazi kwenye bidii yetu, Mithali 10:4 "Atendaye mambo kwa mkono mlegevu huwa maskini;Bali mkono wake aliye na bidii hutajirisha." Unaona sasa kumbe kinachokosekana ni bidii na kujikana.
Hebu dhamiria sasa bila kuangalia kwamba muda umekwenda sana kwamba bado unaweza kufikia mahali ambapo ikifikia Disemba 2018 utajidharau na kusema ni kweli uliruhusu uvivu na uoga tuu, kwani nakuhakikishia utakuwa umepiga hatua kubwa Kabisa na dhamira ya mipango na ndoto zako utakuwa umevihuisha kabisa!!
Kataa kuwa na ndoto na mipango iliyokufa!!!
Jumapili, 25 Machi 2018
111: Kama hakusaidii achana naye!
Jumapili, 4 Februari 2018
Mafanikio sio kitu Rahisi!
Ndugu na Rafiki yangu mpendwa salaam!
Ni matumaini yangu kwamba bado upo katika mapambano ya kufikia kile kizuri unachokitaka.
Wengi wetu tumekuwa tukisoma katika vitabu au nadharia mbalimbali zinazotuongoza katika kufikia mafanikio.
Leo hii napenda nikwambie maneno ambayo yumkini hutayapenda sana lakini ndio ukweli wenyewe.
Kufikia mafanikio siyo rahisi kama tunavyosoma nadharia mbalimbali. Viko vizuizi vingi vya kukukatisha tamaa na kukuvunja moyo ili kuhakikisha hufiki kule unako taka ufikie. Hebu mfano angalia jinsi usingizi ulivyomzuri lakini upande wa pili ukilala bila utaratibu fahamu ndoto za mafanikio zitabaki kuwa ndoto. Hapa ni lazima kuudhibiti usingizi. Wataalam wanatufundisha masaa ya kulala kwa afya ni sita pekee, je mwenzangu unalala masaa mangapi kwa siku!? Hapa nikuombe uchukue hatua ya kuudhibiti usingizi na uutumie muda wako vizuri!
Tambua kuwa usingizi ni kizuizi kimojawapo cha mafanikio ingawa upande wa pili usingizi ni mzuri sana.
.........Kwa leo tuishie hapo na tutaendelea wakati ujao.
Mtega GFA
CEO - UjasiriamaliAfya
Jumatatu, 1 Januari 2018
Ni MWISHO WA YOTE!!
Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa makala za UjasiriamaliAfya, UjasiriamaliAfya blog tunakutakia "Heri ya Mwaka Mpya 2018" lakini kwa nini kila tunapomaliza mwaka huwa tunapeana na kutumiana salaam za heri ya Mwaka Mpya!?
Ndugu msomaji ni muhimu kufahamu ni kwa nini kuna masaa,siku,wiki,mwezi na hatimaye mwaka!? Ni makusudi ya Mungu muumbaji wetu kuwepo nyakati na majira, na majira na nyakati zikipita kinakuja kitu kingine kipya kabisa!
Sasa kwa kuanzia hapa sisi nasi leo tutumie muda kidogo kutafakari majira na nyakati. Mwaka 2017 ndio unaishia na inawezekana kuna mipango na mambo mengi ulipanga yafanyike lakini sasa unaona dakika zimebaki kidogo na hakuna matumaini tena.
Hebu fahamu nyakati ngumu, nyakati za huzuni, nyakati za kutofanikiwa na nyakati za machungu sasa zimekaribia kuishia na 2017 yake.
Unachotakiwa kufanya sasa chukua karatasi na kalamu yako kisha orodhesha mipango na mikakati unayotaka kuiendea mwaka 2018 kwani huo mwaka 2018 ni zawadi kwetu na mambo ni mapya kabisa.
Tangu mapema sahau kushindwa kwako kwa 2017 na tambua 2018 ni nafasi mpya tumepewa. Ukianza bila mipango utaufunga mwaka bila tathimini.
Kumbuka nidhamu ya kujituma, na bidii zaidi katika mipango yako ya 2018.
2018 na uwe wa heri na mafanikio makubwa makubwa kwako!!!!!!
Asante sana!
Mtega George
CEO - UjasiriamaliAfya