Jumapili, 4 Februari 2018

Mafanikio sio kitu Rahisi!

Ndugu na Rafiki yangu mpendwa salaam!
Ni matumaini yangu kwamba bado upo katika mapambano ya kufikia kile kizuri unachokitaka.
Wengi wetu tumekuwa tukisoma katika vitabu au nadharia mbalimbali zinazotuongoza katika kufikia mafanikio.
Leo hii napenda nikwambie maneno ambayo yumkini hutayapenda sana lakini ndio ukweli wenyewe.
Kufikia mafanikio siyo rahisi kama tunavyosoma nadharia mbalimbali. Viko vizuizi vingi vya kukukatisha tamaa na kukuvunja moyo ili kuhakikisha hufiki kule unako taka ufikie. Hebu mfano angalia jinsi usingizi ulivyomzuri lakini upande wa pili ukilala bila utaratibu fahamu ndoto za mafanikio zitabaki kuwa ndoto. Hapa ni lazima kuudhibiti usingizi. Wataalam wanatufundisha masaa ya kulala kwa afya ni sita pekee, je mwenzangu unalala masaa mangapi kwa siku!?  Hapa nikuombe uchukue hatua ya kuudhibiti usingizi na uutumie muda wako vizuri! 
Tambua kuwa usingizi ni kizuizi kimojawapo cha mafanikio ingawa upande wa pili usingizi ni mzuri sana.

.........Kwa leo tuishie hapo na tutaendelea wakati ujao.

Mtega GFA
CEO - UjasiriamaliAfya

Hakuna maoni: