Mpendwa
Msomaji wa makala za “ujasiriamaliafya”, Salaam!
Baada
ya salaam napenda leo tuangalie eneo moja la ni yupi rafiki wa muhimu na yupi
si rafiki wa muhimu. Kwanza kabisa ni muhimu kufahamu kila binadamu anayo
thamani kubwa sana kwa kuwepo kwake hapa duniani ingawa si kila binadamu
anaweza kuwa rafiki yako. Neno rafiki au kiingereza “friend” ni mtu ambaye kwa
namna yeyote atakuwa ni mtu wako wa karibu katika furaha na huzuni. Atakuwa ni
mtu anayependa kukuona unafanikiwa na kuendelea mbele. Na hapa haijalishi
kwamba unalingana naye umri au ni mdogo kuliko wewe au mkubwa kuliko wewe.
Rafiki
anaweza kutoka katika kundi lolote iwe kazini, katika eneo lako la biashara au
mahali popote, muhimu kuangalia jee anakidhi vigezo vya kuwa mtu wangu wa
karibu katika dhiki au katika furaha au mawazo yake yananifanya nisonge
mbele!???. Fahamu jambo moja hapa rafiki kwa vigezo tunavyoangalia leo ni zaidi
ya ndugu, mke au mume wako.
Watu
wengi utaona wanatunza namba nyingi sana katika simu zao na utaona hata
kuzipoteza hawako tayari, kwamba wacha niwe nazo tuu. Swali la kujiuliza jee
namba za simu zote ulizozitunza ni za marafiki zako au watu baki tuu!? Kuwa na
kundi kubwa ambalo kimsingi siyo marafiki zako ni kujichelewesha kimaendeleo na
kupoteza muda wako ambao kama ungeutumia vizuri matokeo yangekuwa yakushangaza.
Ili
uweze kwenda kwa kukimbia na siyo kutembea, leo ninakushauri achana na marafiki
wasikuwa wa msaada kwako kwani hao ni mizigo inayokufanya usikimbie katika
mafanikio yako na zaidi waweza kurudishwa nyuma.
Leo
tuchukue muda wa kutafakari umuhimu wa kila unayemuita rafiki yako na kama
hakusaidii mfute na mpotezee kwani hakusaidii!!! Ili kufikia mafanikio makubwa
na malengo ambayo umekuwa ukiota ndoto ya kuyafikia wakati wote, muhimu ni
kupunguza marafiki wasio na msaada kwako. Na baada ya kuwapunguza imarisha na
ongeza nguvu kubwa zaidi ya kuwashikilia hao wachache ambao umetambua ya kuwa ndio
marafiki zako.
Nakutakia
siku njema!
Mtega
GFA
CEO
– UjasiriamaliAfya
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni