Jumatano, 24 Aprili 2019

Soko Huru na Faida Zake.

Soko Huru ni nini!?
Katika hali ya kawaida na inayouchochea uchumi wa eneo lolote ni kuacha bei ya bidhaa ipangwe na soko lenyewe.
Soko linapangaje bei!?
Kwanza mzalishaji huzalisha akitegemea kuuza kwa faida yaani gharama zote za uzalishaji zirejeshwe na ziada. Ukianza kuuza mazao yako pale utakapoona uhitaji wa bidhaa zako ni mkubwa sana ndipo unaongeza uzalishaji ili kuwafanya wateja wako wapate bidhaa yako pasipo shida. Na katika kuongeza uzalishaji pia unaweza kuongeza bei ili kupunguza wateja wasiolazima ili ujue vyema idadi ya wateja wako na ujipange kuzalisha kile kitakachowakidhi wateja hao.
Soko huru husaidia suala la kupunguza bei na au kuongeza bei kuwa chini ya muuzaji na mnunuaji pekee.

Hakuna maoni: