Jumamosi, 15 Julai 2017

Vitu vinavyoangusha TAASISI!

Taasisi kushindwa, au kufanya vibaya kama ilivyo kwa mtu mmoja mmoja. Vipo visababishi vya msingi na kwa visababishi hivi, wewe kama kiongozi / mtawala au meneja ni vema ukavifahamu na kuchukua tahadhari ili usishindwe kama hao wengine walivyoshangaa kuona ghafla Taasisi iliyokuwa imara inaanguka kwa muda usiotarajiwa. Visababishi hivyo ni:-
1.kutumia nguvu kubwa na msisitizo mkubwa kwa matokeo ya muda mfupi kwa gharama za utafiti na Maendeleo.
2.kushindwa kutumia fursa na uwezo uliopo, na kushindwa kubaini changamoto dhidi ya Taasisi yako.
3.kupuuzia mbinu za kiutendaji.
4.Kuweka nguvu na msisitizo katika kuzalisha na ubunifu wa kihuduma na siyo zaidi katika ubunifu wa mifumo ya Taasisi pamoja na uboreshaji wa huduma za Taasisi.
5.kupuuzia uwekezaji wa mtaji na rasilimali watu.
6.mawasiliano yasiyo mazuri ndani ya Taasisi na ushirikiano usiomzuri baina ya vitengo ndani ya Taasisi.
7.kutofikiria matarajio na mahitaji ya wateja wa Taasisi. Ufunguo wa mafanikio hapa ni kubainisha mahitaji ya wateja wa Taasisi na kuweka nguvu katika kutimiza matarajio yao. Matarajio ya wateja wa Taasisi ni yapi!? Namna gani tutatimiza matarajio yao!?
Mbinu bora za kiutendaji ni lazima ziende sambamba na kutafuta masoko ya bidhaa ya Taasisi kwa wateja wakubwa na au eneo ambalo Taasisi imeamua kulihudumia.
Kufahamu changamoto mbalimbali zitakufanya meneja, kiongozi/mtawala kubuni mbinu ambazo zinawezekana kabisa kuifanya Taasisi yako iwe hai wakati wote.

Asante,

CEO - "ujasiriamaliafya"

Hakuna maoni: