SEHEMU YA KWANZA: MLO
KAMILI.
Utangulizi.
Ujasiriamali unategemea sana uimara wa afya yako. Ni kwa msingi huo leo tutaangalia muongozo wa ulaji kwa watu waishio na UKIMWI/WAVIU.
Lishe ni mahitaji ya msingi kwa binadamu
wote. Magonjwa sugu huzuia mmeng’enyo wa wa chakula mwilini, husababisha mtu
kukosa hamu ya kula na hivyo kusababisha utapiamlo. Kwa WAVIU na magonjwa
mengine sugu,mahitaji ya lishe kwenye mwili ni makubwa wakati dalili za mwanzo
hazijaanza kuonekana. Hatari yakupata utapiamlo inaongezeka katika kipindi cha
ugonjwa. Lishe bora siyo tiba bali ni kinga dhidi ya maambukizo. Lishe bora
huongeza kinga pamoja na ubora wa maisha.
Nini maana ya mlo kamili?
Jibu: Mlo kamili ni
ule wenye mchanganyiko wa vyakula kutoka makundi mbalimbali. Mlo huo huwa na
virutubishi vyote muhimu na kwa kiasi kinachotosheleza kwa afya bora ya mlaji.Ni
muhimu sana vyakula hivi viliwe kwa wakati mmoja ili kuuwezesha mwili kutumia
virutubishi mbalimbali kwa ufanisi. Kwa mfano, Vitamini C husaidia ufyonzwaji wa madini ya chuma yanayo patikana kwenye vyakula vyenye asili ya
mimea, pia mafuta husaidia
ufyonzwaji wa vitamin A, D,E na K. Hakikisha kwamba milo miwili(2) hadi mitatu(3)
kwa siku iwe milo kamili.
Maana
ya Lishe:
Lishe
ni sayansi ya matumizi ya virutibisho kwenye mwili wa binadamu kwa ajili ya
maendeleo, ukuaji, uzalishaji na utunzaji wa afya.
Kwa
nini ule mlo kamili?
Ø
Huwezesha
mwili kupata virutubishi vyote vinavyohitajika kwa wakati mmoja.
Ø
Huboresha
kinga ya mwili dhidi ya maradhi mbalimbali.
Ø Humpa
mtu nguvu za kufanya kazi mbalimbali.
Ø Huuwezesha
mwili kutumia virutubishi mbalimbali kwa ufanisi. Kwa mfano, Vitamini C husaidia ufyonzwaji wa madini ya chuma yanayo patikana kwenye vyakula vyenye asili ya
mimea, pia mafuta husaidia
ufyonzwaji wa vitamin A, D,E na K.
KUMBUKA:
Tumia
vyakula vinavyopatikana kwenye mazingira unayoishi.
Ø Tumia
vyakula vya asili ikiwa ni pamoja na mboga-mboga, matunda pori na wadudu
wanaoliwa.
Ø Kula
matunda na mboga-mboga katika kila mlo.
Ø Badili
aina ya vyakula kila inapowezekana.
Ø Chakula
cha kutosha huuwezesha mwili kukidhi ongezeko la mahitaji ya virutubishi.
Ø Kula
milo miwili(2) hadi mitatu(3) iliyo kamili na asusa (vitafunwa) kati ya mlo na
mlo.
Ø Kula
milo midogo midogo mara nyingi, endapo huwezi kula chakula cha kutosha kwa mara
moja.
Ø Zingatia
usafi na usalama wa chakula na maji.
Ø Tumia
mafuta na sukari kwa kiasi.
Ø Punguza
matumizi ya chumvi.
Ø Kahawa, kokoa, chai, chokoleti na baadhi ya
soda vina kafeini ambayo huzuia ufonzwaji wa madini ya chuma yanayopatikana
kwenye vyakula vya mimea.
Ø Mtu mwenye VVU/ UKIMWI inapobidi anaweza
kutumia kwa kiasi kidogo angalau saa moja kabla au baada ya kula.
Ø Epuka
kutumia pombe na sigara kwa sababu vinaingilia matumizi ya chakula na
virutubishi, na pia huchangia kupunguza kinga ya mwili. Kadhalika hukuongezea
hatari ya kupata magonjwa sugu kama saratani ya kinywa, koromeo na ini na hata
kifua kikuu.
Ø Fanya
mazoezi ya mwili kama shuguli za nyumbani, kazi za bustani au kutembea ili
kuboresha matumizi ya chakula mwili na kujenga misuli.
Ø Aina
ya mazoezi hutegemea hali ya mgonjwa.
SEHEMU YA PILI.
Mlo kamili unatakiwa kuwa na chakula
angalau kimoja kutoka katika makundi yafuatayo ya vyakula na vyakula hivyo viliwe
pamoja.
1 .KUNDI LA KWANZA
Nafaka,
mizizi na ndizi
za kupika.
·
Mazao ya nafaka ni; mahindi, ulezi,
ngano, mtama,mpunga, uwele na shayiri.
·
Mazao ya mizizi ni; viazi vitamu, viazi mviringo, viazi vikuu, magimbi, mhogo na
vyakula vingine vingi vya mizizi.
·
Ndizi mbichi za kupika ambazo hazijaanza
kuiva.
Vyakula vya kundi hili
huchukua sehemu kubwa ya mlo ambapo kazi yake kubwa ni kuupa mwili nguvu na joto, pia huupa mwili kiasi kidogo
cha madini, vitamini na utomwili ( protini ).
2. KUNDI LA PILI.
Vyakula
vya jamii ya mikunde, vile vyenye kokwa na vyenye asili ya wanyama:
Jamii
ya mikunde ni;
·
Maharage, njegere, kunde; soya,
njugumawe, dengu, mbaazi, fiwi na choroko.
Vyenye
kokwa ni;
·
Karanga,
korosho, kweme na kokwa za asili zinazo toa mafuta.
Vyemye
asili ya wanyama ni;
·
Nyama,
samaki, dagaa, senene, maziwa, jibini, mayai, nzige na kumbikumbi na wadudu wengine
wanaoliwa. Vyakula vya kundi hili huupatia mwili utomwili (protini ) na kiasi kidogo
cha vitamini na madini.
·
Kazi ya protini ni kukarabati na kukuza
mwili.
3. KUNDI LA TATU.
Mboga-mboga:
·
kundi
hili linajumuisha aina zote za mboga za majani (mboga za kupandwa na mboga
pori) kama mchicha, matembele, majani ya kunde, majani ya maharage, mnafu,
mchunga, bamia, pilipili hoho, karoti, bilinganya, maboga, matango, bitiruti na
mboga mbalimbali za asili.
- Mboga-mboga huupatia mwili vitamini na madini kwa wingi ambavyo kazi yake kubwa sana ni kuboresha kinga ya mwili hasa kwa watu wanaoishi na VVU /UKIMWI
4.KUNDI LA NNE.
Matunda:
- Kundi hili linajumuisha aina zote za matunda kama pera, papai, embe, chungwa, karakara (pesheni ), limau, ndimu, chenza, parachichi, ndizi mbivu, nanasi, pichesi, stafeli, fenesi, zambarau, topetope na matunda pori yaliwayo kama vile ukwaju, ubuyu, mabungo, embe ng’ong’o, nk.
5. KUNDI LA TANO.
Mafuta na Sukari.
Mafuta na sukari
huongeza nishati-lishe (nguvu) na uzito wa mwili, pia huupa mwili joto. Vyakula
hivi pia huongeza ladha ya vyakula. Pia mafuta hulainisha vyakula na kusaidia
uyeyushwaji na usharabu wa baadhi ya virutubishi kama A, D, E na K. Vyanzo vya
mafuta ni:
Mafuta yatokanayo na mimea
ni:
· Korosho,
ufuta, alizeti, kweme, karanga, nazi, mbegu za maboga, mafuta ya mawese na mbegu
za mimea ya porini.
Mafuta
yatokanayo na wanyama:
·
Samli,
siagi, mafuta ya nyama yenyewe na mafuta ya samaki.
Sukari:
·
Sukari
yenyewe, sukari gulu, miwa na asali.
Maji.
Japo siyo kundi la chakula lakini ni
sehemu muhimu ya mlo. Maji ni muhimu kwa kurekebisha joto la mwili na kusaidia
mfumo wa chakula. Ili mwili ufanye kazi yake vizuri kwa uhai unahitaji uwepo wa
maji. Nimuhimu kunywa maji angalau lita 1.5(glasi 8) kwa siku. Ni muhimu sana kunywa
maji safi na salama.
MFANO
WA RATIBA YA MLO KAMILI KWA WAVIU.
MUDA WA KULA CHAKULA
|
AINA YA CHAKULA
|
||
1
|
Saa 1: 30 Asubuhi.
|
Uji wa mahindi uliochanganywa karanga na dagaa.
|
|
|
|
|
|
2
|
Saa
4: 30 Asubuhi.
|
Chai, yai la kuchemshwa, parachichi na
viazi vilivyoungwa karanga.
|
|
|
|
|
|
3
|
Saa 7: 30 Mchana.
|
Ugali wa mahindi, Njegele, Mboga ya
matembele imeungwa kwa mafuta ya alizeti, Parachichi.
|
|
|
|
|
|
4
|
Saa 10: 30 Mchana.
|
Karanga zilizo kaangwa za kutafuna na
maji ya matunda.
|
|
|
|
|
|
5
|
Saa 1: 30
Usiku
|
Ndizi
zilizo pikwa pamoja na bamia na nyama,
Mchicha, Chungwa.
|
|
|
|
|
|
6
|
Saa 4: 00 Usiku
|
Kachumbali.
|
Hakikisha
kwamba milo miwili(2) hadi mitatu(3) kwa siku iwe milo kamili.
Pamoja
na ulaji bora uliotajwa hapo juu mgonjwa au mtu anayeishi na VVU anapaswa
kufanya yafuatayo:
a. Aepuke
kupata maambukizo mapya.
b. Aepuke
kuwaambukiza watu wengine.
c. Afanye
kazi za kipimo/asifanye kazi ngumu.
d. Apate
mapumuziko ya kutosha.
e. Afanye
mazoezi ya viungo kwa kutembea n.k.
f. Asitumie
pombe aina yoyote wala kuvuta sigara.
g. Azingatie
usafi wa mwili, mavazi, mahali pa kulala na mazingira yake.
h. Anywe
maji safi na salama.
i.
Ashiriki shughuli mbalimbali za kijamii,
kiuchumi na maendeleo.
Imendaliwa
na;
Leslie Mhagama
0763 90 10 46
lesliemhagama@gmail.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni