Jumapili, 27 Agosti 2017

AFYA YA UZAZI KWA VIJANA



     SOMO: KWA NINI ELIMU YA KINA YA UJINSIA, MAADILI YA AFYA NA STADI ZA MAISHA [Comprehensive Sexuality Education – CSE]?
Ø  Inawawezesha Vijana balehe kujizuia na mimba zisizotarajiwa na maambukizo kwa njia ya ngono, ikiwa ni pamoja na VVU.
Ø  Inawasaidia Vijana balehe kufanya maamuzi sahihi hasa ya kuchelewa kuanza kufanya ngono na ukatili wa kijinsia.
Ø  Ina hamasisha Vijana balehe kuwa na uhusiano unaofaa zaidi na wenye Afya pamoja na kupunguza ukatili wa kijinsia, uonevu na ubaguzi.
KWA NINI HUDUMA ZA UJINSIA NA AFYA YA UZAZI – Sexuality Reproductive Health?
Vijana balehe wanahitaji kupata elimu salama, za gharama nafuu na zinazokubalika kulingana na viwango vya Kimataifa vya Huduma Rafiki za Afya ya Uzazi kwa Vijana.
Serikali zinawajibu wa kutoa huduma hizi kwa sababu:
Ø  Kutimiza haki ya afya ya umma kulinda afya ya kizazi kijacho.
Ø  Zitolewe kwa pamoja na huduma nyingine za elimu ya ujinsia, afya ya uzazi, maadili ya afya na stadi za maisha zenye ufanisi zaidi.
Ø  Kuhakikisha kwamba Vijana balehe wanajisikia salama na kujiamini katika upatikanaji wa huduma.
Ø  Kupunguza mimba zisizotarajiwa, VVU, magonjwa mengine ya ngono na kuboresha kiwango cha kuishi kwa wajawazito na watoto hatimaye kuliletea Taifa letu maendeleo makubwa sana.


                                        VIJANA WA LEO.
HALI HALISI YA AFYA YA UZAZI KWA VIJANA TANZANIA
VIJANA NI IDADI KUBWA YA WANANCHI TANZANIA
UJANA ni umri kati ya miaka 10 hadi 24. Ni kipindi cha mpito kati ya utoto na utu uzima ambapo vijana wanapitia mabadiliko mengi ya ukuaji na kiafya.
RIPOTI YA TAFITI ZA DEMOGRAFIA NA AFYA ZA 2010.
·         Tanzania ilikuwa na jumla ya watu milioni 43.2 [ 43,187 823 ], Vijana milioni 14 = 31%

MATATIZO YA VIJANA YA AFYA YA UZAZI

1.    Wasichana wengi huanza kujihusisha na ngono kwa wastani wakiwa na umri wa miaka 17 wakati wavulana miaka 15
2.    Vijana wengi huanza kujihusisha na mapenzi kabla ya kuingia kwenye ndoa.
3.     32% ya wasichana wasioolewa na wavulana  42% wasiooa wa umri wa miaka  14 -20 walishaanza kujamiana.
4.    9% ya wasichana na 10% ya wavulana wa miaka 15 – 20 walishaanza kujamiana kabla ya kutimiza umri wa miaka 15.
5.    Inakadiriwa kuwa  65% ya wasichana wafikapo umri wa miaka 18 tayari huwa wameshaanza kujamiiana.
6.    18% ya wasichana wenye umri  wa  miaka 15 – 19 tayari                                                                wameshaolewa na 37% ya wasichana wenye umri wa miaka 20 – 24 waliolewa   au kuwa kwenye unyumba walipokuwa na umri wa      miaka 18.
7.    4% ya wavulana wenye umri kati ya miaka 15 -19 wameshaoa. Ndoa za utotoni hutokea kwa kiwango kikubwa katika Mikoa ya Shinyanga ambapo 59% ya wasichana wenye umri wa miaka 15 -19 walishaolewa na mkoa wa Mara ni 55%.Kuolewa katika umri chini ya miaka 20 ni kuwaweka wasichana katika hatari ya kupata mimba za utotoni.
                                     
Ø  Mimba katika umri mdogo ni tatizo kubwa mojawapo la Afya ya Uzazi hapa nchini.
Ø  23% ya wasichana wenye umri wa miaka 15 – 19 wamekwisha zaa watoto hai au wana mimba ya kwanza ambapo 6% wana ujauzito wa kwanza.
Ø  Wasichana 116 kati ya 1000 wenye umri kati ya miaka 10 – 19 wana watoto tayari.
Ø  Ni 16% tu ya wasichana wenye umri wa miaka 15 – 24 wanatumia njia za kisasa za uzazi wa mpango.
Ø  22% ya wasichana wanataka kutumia njia za uzazi wa mpango lakini wanashindwa kupata huduma hizo.

WASICHANA KUPATA MIMBA KATIKA UMRI MDOGO

v  Ni tatizo kubwa sana la afya ya uzazi nchini.
v  23% ya wasichana wenye umri wa kati ya 15 -19 wamekwisha zaa mtoto hai au wana mimba.
v  52% ya wasichana wenye umri wa miaka 15 -19 hawana elimu ya sekondari kutokana na kuapata mimba ama watoto.
v  Mimba za utotoni huchangia vifo vingi vya wajawazito na watoto.
v  Watoto waliozaliwa na wasichana wenye umri mdogo wananafasi    ndogo ya kuishi kufikia miaka 5 ikilinganishwa na wale wanao               zaliwa na wanawake wenye umri mkubwa.
v  Wasichana 111 kwa 1000 wenye umri chini ya miaka 20 hupoteza watoto wao tofauti na vifo vya watoto waliozaliwa na wanawake wenye umri  kati ya miaka 30 hadi 39 ambapo ni 93 kwa 1000.

UTOAJI MIMBA.
Vifo ni 16%, wengi wao ni vijana.

MATATIZO YA KUJAMIIANA KATIKA UMRI MDOGO.

Kwa Msichana
A.   Kukatiza masomo na kuathirika kimaisha.
B.   Kukataliwa na familia.
C.   Kupata matatizo wakati wa kujifungua.
D.   Kifo
Kwa Mvulana:
A.   Kukatiza masomo na kuathirika kimaisha.
B.   Kufunga ndoa za kulazimishwa.
C.   Kukosa uwezo wa kulea familia.
Kwa mtoto:
Ø  Kuzaliwa na uzito pungufu.
Ø  Kuzaliwa mtoto njiti.
Ø  Kupata matatizo wakati wa kuzaliwa
Ø  Kukosa mapenzi kwa wazazi.
Ø  Kifo

VIJANA NA MAAMBUKIZO YA VVU/UKIMWI
v  UKIMWI ni ugonjwa unaosababishwa na Virusi Vya UKIMWI [VVU/ HIV] vinavyodhoofisha kinga ya mwili ya kujikinga na maradhi mbalimbali.

JINSI UKIMWI UNAVYOENEZWA.
Ø  90% ya maambukizo ni kwa njia ya kujamiiana na mtu mwenye VVU.
Ø  Mama mwenye VVU anaweza kumwambukiza mototo wake wakati wa:
a.   Ujauzito.
b.   Uchungu na kujifungua.
c.    Kunyonyesha
d.   Kuchangia damu yenye VVU.

ü  Karibu 1/2 ya wasichana na 1/3 ya wavulana wamewahi kupimwa VVU na kupokea majibu yao.
ü   Vijana wa miaka 15 – 24 huchangia kwa 2% ya maambukizi mapya ya VVU Tanzania.
ü  Vijana walio kwenye ndoa au wanaishi na wenza maambukizi ya VVU ni 2.6% ikilinganishwa na 1.4% ya ambao hawako kwenye ndoa.
ü  Maambukizi mapya ya VVU ni 45% kwa wasichana wenye umri kati ya miaka 15 – 24 wakati wanaume ni 26% kwa umri huo.
ü  Magonjwa ya ngono yanaongeza kasi ya maambukizo ya VVU.

MAGONJWA YATOKANAYO NA KUJAMIANA.
Magonjwa yanayo ambukizwa kwa njia ya tendo la kujamiiana na mtu  ni miongoni mwa magonjwa haya;
Ø  Kisonono
Ø  Klamidia
Ø  Trichomoniasis
Ø  Kaswende
Ø  Herpes
Ø  Pangusa – Chancroid
Ø  Virusi Vya UKIMWI

NAMNA YA KUJIKINGA NA MIMBA.
v  Kuacha kabisa kujamiana.
v  Tumia kondomu kila wakati na kwa usahihi.
v  Tumia njia ya uzazi wa mpango uliyoichagua kuzuia mimba.

NAMNA YA KUEPUKA TENDO LA KUJAMIIANA AMBALO SI SALAMA NA SI LAZIMA KWA WASIO NA NDOA.
ü  Epuka kujamiiana katika umri mdogo, kama ulishaanza acha mara moja.
ü  Epuka ulevi wa aina yoyote ile
ü  Shiriki katika michezo mbalimbali ili kupambana na mihemko ya mwili wako.
ü  Endapo utashindwa kujizuia kabisa unashauriwa kutumia kondomu kwa usahihi.
ü  Kondomu ikitumika kwa usahihi kwa kila tendo la kujamiiana huzuia mimba, maambukizo ya VVU na  magonjwa ya ngono.
ü  Epuka kushirikiana na rafiki mpenda ngono,kuomba omba/  kupewa zawadi mbalimbali na vishawishi vingine vingi ambavyo vitasababisha uingie katika ngono.
ü  Usifanye rushwa ya ngono, ni kosa la kisheria.
ü  Epuka tabia ya uvivu.
ü  Usishiriki michezo na mikesha ya usiku isiyo ya lazima.
ü  Enzi Mafundisho ya dini yako kwani ni mafundisho yanayo kataza zinaa.

TAHADHARI kwa Wasichana:
     Wanaweza kupata mimba
v  Kabla ya kupata hedhi.
v  Bila kufanya tendo la kujamiiana endapo katika hali ya mapenzi mvulana atamwaga shahawa karibu na UKE.
v  Wanapofanya tendo la kujamiiana kwa mara ya kwanza.
           
NJIA ZA UZAZI WA MPANGO:
a] Za muda mfupi:
      > Vidonge vyenye Vichocheo Viwili
      >      ,,              ,, kichocheo kimoja [POPS]
     > Dawa Za Povu Na Jeli [Spermicides]
      > Njia ya Ute [BOM]
      > Kunyonyesha Tu [LAM]

b] Za muda mrefu:
     > Sindano [ Depo Provena ]
     > Vipandikizi [ Norplant ]
     > Kitanzi [ IUCD ]
AFYA YA UZAZI NA MALEZI KWA VIJANA BALEHE.

C] Njia za kudumu:
      > Kufunga uzazi mwanaume [ Vasectomy ]
      > Kufunga uzazi mwanamke  [ BTL ]

Marejeo:           
1.    Youth in Tanzania – data from the 2010 Tanzania Demographic and Health Survey ( TDHS ).
2.    Vijana Wa Leo handouts – Wizara ya afya na U/Jamii.
3.    National Adolescent Reproductive Health Strategy 2011 – 2015.
4.    Wizara ya Afya na U/Jamii, Kitengo Cha Afya ya Uzazi na Mtoto, barua pepe:Afya_promo@moh.go.tz
      

Hakuna maoni: