Jumatano, 1 Novemba 2017

Akili yako ndio mtaji wako!!!

"Ni kipi kinachemka ndani yako"!???
Mpendwa msomaji,
Ni muhimu kufahamu kila binadamu anachokitu ndani mwake chenye msukumo mkubwa kukifanya na wakati mwingine kinakupa majibu kuwa hii ndiyo dili itakayo nifanya nifanikiwe. Sauti hiyo kamwe usipuuze ikiwa tuu unaliona ni jambo jema!!!.
Katika hali ya asili ya mwanadamu ya kawaida utaona iko sauti nyingine inayokuja ikiwa na nguvu kuliko Ile ya kwanza na itakuletea vikwazo vingi sana! Nasema ipuuze sauti hiyo, kwani haikutakii mema bali ni sauti ya maadui wa maono yako!
Kadhalika usitegemee watu utakao waingiza kukusaidia kukufikisha unakotaka kwenda kuwa watakufikisha sawasawa na utakavyo ikiwa hauna usimamizi mzuri. Kwakuwa wewe ndiye uliyebeba ramani ya biashara au shughuli zako, hivyo usitegemee wasaidizi wako wanaweza kukufikisha kule unakotaka kufikia ikiwa hauna uangalizi wa karibu. Na pia hujaweka dhibiti/controls za malengo yako.
Fahamu tabia ya taasisi yako inategemea sana namna unavyosimamia kwa umakini ramani yako. Hivyo endelea kujihoji, 'hiki kinachoendelea ndiyo ramani yangu'!? Ikiwa jibu ni 'siyo' chukua hatua za kukiondoa. Na endelea na umakini huo tena na tena maana ndivyo utakavyofikia kilele cha mafanikio yako!

Nimalizie kwa kusema "akili yako ndiyo mafanikio yako" !

Hakuna maoni: