Watu wengi wanapenda kuwa mbele ya wengine yaani kuwa viongozi. Kupenda huko ni jambo jema sana! Mpendwa msomaji wa makala za "ujasiriamaliafya.blogspot.com" kabla ya kutamani kuwa katika nafasi hiyo fahamu kanuni hii "huwezi kwenda juu sana bila kuacha" yeyote aliyefanikiwa kuwa juu sana kwanza alizingatia kanuni hii, "kujikana" Kwa kuacha baadhi ya mambo fulani na kuongeza bidii zaidi katika jambo lile alilolikusudia kwamba litamfanya awe mbele ya wengine.
Kiongozi bora vivyo hivyo ni yule anayeacha mambo yake binafsi na kujitaabisha kwaajili ya wengine. Ataangalia kero na changamoto za wale waliomzunguka au wale anaotaka kuwaongoza na kutafuta njia sahihi ya kuwatoa pale walipo na kuwapeleka kwenye matarajio yao.
Katika mazingira hayo utaona mambo yahusuyo familia yako na mambo yako binafsi yanapewa uzito kidogo kuliko yale ya watu wengine. Dunia ya leo inakosa watu wa namna hii kwa wingi kwani wengi hutamani kuongoza kwa nia ya kujitajirisha au kutafuta faida binafsi.
Jee unatamani kuwa kiongozi bora!? JIKANE NAFSI YAKO NA KUANGALIA YA WENGINE!
Jumapili, 25 Juni 2017
KUJIKANA, SIFA YA KIONGOZI!
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni