Jumamosi, 25 Machi 2017

Tafakari ya Robo Mwaka!

Mpendwa msomaji na rafiki yangu wa "ujasiriamaliafya.blogspot.com" kwanza kabisa nikupongeze kwa kufuatilia kwa umakini makala zetu! Nina hakika yapo mafanikio makubwa umeanza kuyaona katika maisha yako kwa hatua yako ya kuwa mtekelezaji wa maarifa hayo na si msomaji tuu! Hongera sana! Lakini Leo tuangalie na kila mmoja ujipime binafsi, tangu mwaka uanze tunakaribia kumaliza robo mwaka. Je shauku na Mipango yako kwa mwaka huu umejitathmini na kuona vinalingana na kalenda ya Mwaka huu kama ulivyokuwa umepangilia Mwanzoni mwa Mwaka au bado kuna vikwazo!? Jee muda wa miezi mitatu, fedha za miezi mitatu, uhai wa miezi mitatu, n.k umevitumia kwa matokeo yanayoonekana na kushikika yaani "tangible"!? Kama jibu lako ni  ndivyo, Hongera sana! Hata hivyo nikukumbushe rafiki yangu, usibweteke kwa yale uliyokwisha fanya tayari bali ongeza jitihada zaidi ili miezi mingine mitatu ijayo tuone tutakuwa tumefikia wapi!? Kumbuka mafanikio ni safari isiyo na mwisho na inahitajika bidii hivyo basi nakushauri endelea mbele huku ukijitahidi kusahau uliyokwisha kuyafanya na kujiona kana kwamba ndio unaanza sasa ndivyoutakavyo fanya makubwa zaidi, kwani hakika tukitumia rasilimali zilizotuzunguka kwa umakini, nina kuhakikishia mambo mazuri zaidi yapo mbele yako!!!

Hakuna maoni: