Ulishaji
Kuku kama mifugo mingine uhitaji chakula chenye virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini ili kukua upesi na kuwa na na afya nzuri . Chakula kinachofaa ni mchanganyiko wa viini lishe mbalimbali vyenye kazi tofauti mwilini. Kila kiini lishe hakina budi kiwe katika kiwango sahihi kulingana mahitaji ya mwili wa kuku katika umri tofauti.
Kuku kama mifugo mingine uhitaji chakula chenye virutubisho vyote vinavyohitajika mwilini ili kukua upesi na kuwa na na afya nzuri . Chakula kinachofaa ni mchanganyiko wa viini lishe mbalimbali vyenye kazi tofauti mwilini. Kila kiini lishe hakina budi kiwe katika kiwango sahihi kulingana mahitaji ya mwili wa kuku katika umri tofauti.
Kuku anahitaji chakula chenye viini lishe vifuatavyo:
Kiini
lishe
|
Kinapatikana
katika chakula gani
|
Kazi
yake mwilini
|
Wanga
|
Pumba,Chenga
za nafaka kama
mahindi,
mtama.
|
Kutia
nguvu mwilini
|
Mafuta
|
Mashudu
yanayopatikana baada ya
kukamua
mbegu za mafuta kama
alizeti,
karanga n.k
|
Kutia
nguvu na joto
mwilini
|
Protini
|
Mashudu
ya karanga au alizeti.Damu
iliyokaushwa
ya wanyama kama
mbuzi,
ng’ombe n.k. Mbegu za jamii
ya
mikunde kama maharage, kunde,
soya....
|
Kujenga
mwili na
kukarabati
mwili
|
Vitamini
|
Majani
mabichi kama mabaki ya
mboga za
majani, michicha ya porini,
majani
mabichi ya mipapai, majani ya
Lusina
n.k.
|
Kulinda
mwili. Majani
mabichi
pia huwezesha
kuku
kutaga mayai yenye
kiina
cha njano, rangi
ambayo
huwavutia walaji
wengi.
|
Madini
(calsium
na
Fosforas)
|
Unga wa
dagaa, unga wa mifupa
iliyochomwa,
chokaa
|
Kujenga
mifupa,
kutengeneza
maganda
ya
mayai
|
Mfano wa kuandaa vyakula vya makundi tofauti ya kuku
Kwa Vifaranga
Kwa vifaranga vya tangu kutotolewa hadi miezi miwili tengeneza mchanganyiko ufuatao.Huu ni mfano mmojawapo wa kuandaa kilo 100 za chakula cha vifaranga. Iwapo utahitaji kuandaa jumla ya kilo 50 za chakula tumia nusu ya vipimo vilivyoainishwa katika jedwali hili.
Wastani wa mahitaji ya kuku wakubwa 50 kwa siku ni kilo 5. Chakula hiki ukigawe katika sehemu mbili na kuwapatia nusu asubuhi na nusu ya pili mchana.
Vifaranga hupewa chakula kiasi wanachoweza kumaliza (hawapimiwi).
Vifaa
|
Kiasi kwa kilo
|
Dagaa
(unga au vichwa vya dagaa)
|
12
hadi 15
|
Chenga
za nafaka kama mahindi au mtama n.k
|
40
|
Mashudu
|
20
|
Pumba
|
24
|
Chokaa
|
2
|
Unga
wa Mifupa,Madini ( Premix)
|
2
|
Chumvi
|
Robo
kilo
|
Mchanga
|
1
|
Jumla
|
Kilo
100
|
Kwa kuku wanaokua (baada ya miezi miwili ).
Vifaa
|
Kiasi kwa kilo
|
Dagaa
(unga au vichwa vya dagaa)
|
7
|
Chenga
za nafaka kama mahindi au mtama n.k
|
30
|
Mashudu
|
20
|
Pumba
|
39
|
Chokaa
|
2
|
Unga
wa Mifupa,Madini ( Premix)
|
2
|
Chumvi
|
Robo
kilo
|
Mchanga
|
1
|
Jumla
|
Kilo
100
|
Kama umeamua kufuga kuku kwa mtindo wa kuwaacha huru wajitafutie chakula (huria) unaweza kuwapatia vifaranga nyongeza ya protini.Utafanya hivyo kwa kuwachanganyia vumbi au vichwa vya dagaa kiasi cha kikombe kimoja vilivyotwangwa pamoja na pumba ya mahindi vikombe vitano.
Maji ya Kunywa
Mfugaji ahakikishe anawapatia kuku maji masafi ya kunywa na ya kutosha kila siku.Vyombo vya maji ya kunywa budi visafishwe vizuri kila siku. Hii itasaidia sana kudhibiti magonjwa yanayoweza kutokana na vimelea vya magonjwa vinavyostawi katika maji yasiyo safi. Kuku wanaweza kuwekewa maji katika aina tofauti ya vyombo kutegemea na urahisi wa kupatikana mfano sufuria, ndoo za plastik zilizokatwa kuruhusu kuku kunywa bila kuchafua.
Mfugaji ahakikishe anawapatia kuku maji masafi ya kunywa na ya kutosha kila siku.Vyombo vya maji ya kunywa budi visafishwe vizuri kila siku. Hii itasaidia sana kudhibiti magonjwa yanayoweza kutokana na vimelea vya magonjwa vinavyostawi katika maji yasiyo safi. Kuku wanaweza kuwekewa maji katika aina tofauti ya vyombo kutegemea na urahisi wa kupatikana mfano sufuria, ndoo za plastik zilizokatwa kuruhusu kuku kunywa bila kuchafua.
Usafi katika banda
Matandazo yanayowekwa katika sakafu ya banda la kuku hayana budi yageuzwe mara kwa mara kwa wastani wa kila baada ya miezi miwili au mitatu . Wakati mwingine ni kabla ya kipindi hiki muda wowote yanapoloana na maji. Matandazo uharakisha kukauka kwa unyevu katika banda unaotokana na kinyesi cha kuku na pia zaidi na maji yanayomwagika.
Matandazo yanayowekwa katika sakafu ya banda la kuku hayana budi yageuzwe mara kwa mara kwa wastani wa kila baada ya miezi miwili au mitatu . Wakati mwingine ni kabla ya kipindi hiki muda wowote yanapoloana na maji. Matandazo uharakisha kukauka kwa unyevu katika banda unaotokana na kinyesi cha kuku na pia zaidi na maji yanayomwagika.
Usafi katika banda utasaidia kudhibiti kwa kiasi kikubwa magonjwa mbalimbali.
Kuokota mayai
Usiyaache mayai ndani ya viota kwa muda mrefu, yaokote mara kwa mara ili kuepuka kuharibiwa kwa mayai hayo na kuku wenyewe. Kuku wanayo tabia ya kula mayai yao ikiwa chakula unachowapa kina upungufu wa protini.
Usiyaache mayai ndani ya viota kwa muda mrefu, yaokote mara kwa mara ili kuepuka kuharibiwa kwa mayai hayo na kuku wenyewe. Kuku wanayo tabia ya kula mayai yao ikiwa chakula unachowapa kina upungufu wa protini.
Vilevile kiasi cha mwanga unaoingia ndani ya banda kikizidi kuku hula mayai au kudonoana wenyewe kwa wenyewe.Uonapo dalili za namna hii kwenye kundi lako punguza kiasi cha mwanga kwa kuziba sehemu za madirisha kwa vipande vya magunia au vipande vya makasha ya karatasi ngumu.
Kama ilivyoelezwa awali kuku wapewe majani mabichi ya kutosha mara kwa mara ili wawe wanakula hayo badala ya kudonoana. Pia fuatilia kuhakikiksha kama chakula kina protini ya kutosha. Kama tatizo la kudonoana na kula mayai litaendelea omba msaada kwa mtaalam wa mifugo akuelekeze jinsi ya
kuwakata au kuwachoma midomo.
kuwakata au kuwachoma midomo.
Source: RLDC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni