Magonjwa ya Kuku
Magonjwa ya kuku yapo mengi. Hata hivyo siyo yote yanatokea mara kwa mara hapa Tanzania. IIi uweze kudhibiti yale yanayotokea katika kundi lako unahitaji kufahamu dalili za jumla za magonjwa hayo. Unapoigundua moja au zaidi ya dalili za ugonjwa au wadudu chukua hatua mara moja. Yapo magonjwa ambayo yanaweza kuangamiza kundi lote la kuku katika muda mfupi.
Magonjwa ya kuku yapo mengi. Hata hivyo siyo yote yanatokea mara kwa mara hapa Tanzania. IIi uweze kudhibiti yale yanayotokea katika kundi lako unahitaji kufahamu dalili za jumla za magonjwa hayo. Unapoigundua moja au zaidi ya dalili za ugonjwa au wadudu chukua hatua mara moja. Yapo magonjwa ambayo yanaweza kuangamiza kundi lote la kuku katika muda mfupi.
Jihadhari na uwezekano wa kupatwa na hasara zinazoletwa na magonjwa ambayo unaweza kuyazuia.
Katika sehemu hii utajifunza kwa muhtasari tu dalili za jumla za magonjwa ya kuku na jinsi ya kuyadhibiti.Dalili za Jumla za Magonjwa ya Kuku
- Kuku kupoteza hamu ya kula.
- Kuzubaa na kukaa mahali pamoja kwa muda mrefu (Kutochangamka).
- Kushuka kwa kiwango cha utagaji wa mayai.
- Vifaranga kutokua upesi au kudumaa. - Macho kuwa na rangi nyekundu.
- Kujikunja shingo.
- Kutetemeka, kutoa majimaji puani, mdomoni na machoni.
- Kutoa mharo (kinyesi) wa rangi ya kijani au wenye mchanganyiko na damu au cheupe.
- Kukonda.
- Kukohoa.
Ukiona moja au zaidi ya dalili hizi katika kundi lako chukua hatua za kutibu zilizoelezwa hapa chini. Kama hali ni ngumu zaidi omba msaada kwa mtaalam wa tiba ya mifugo ili achunguze mara moja na kukushauri jambo la kufanya.
Muhtasari wa Magonjwa Muhimu ya Kuku na Jinsi ya Kuyadhibiti na Kutibu
Ugonjwa
|
Chanzo
|
Dalili
|
Kudhibiti na Kutibu
|
1.
Kideri
(Newcastle)
|
Virusi
|
Kukohoa,
kupumua
kwa
shida.
Mwili
kukosa
nguvu; shingo
kujikunja.
Kuharisha
kijani.
Kuku
hufa wengi
Kuhara
damu.
|
Vifaranga
wachanjwe
katika
juma lao la
kwanza.
Chanjo la pili
wanapofikisha
umri wa
miezi 4
na nusu.
Chanja
kuku kila baada ya
miezi
mitatu.
|
2.
Kuhara damu
(Coccidiosis)
|
Bakteria
|
Kuku
hujikusanya pamoja.
Hawachangamki.
Hushusha
mbawa.
|
• Tunza
usafi katika
banda.
• Lisha
vifaranga chakula
k i l
ichochanganywa
na dawa
ya kinga
coccidiost
kama
Amprolium
au Salfa.
•
Watenge kuku wote
Walioambukizwa
na
wapatie
dawa kama
Amprolium
au salfa au
Esb3.
|
3. Ndui
ya kuku
(Fowl
pox)
|
Virusi
|
Malengelenge
kwenye
kishungi
na kope za
macho na
sehemu zisizo
na
manyoya.
|
•
Kuchanja kuku wote
wakiwa
na umri wa
miezi
miwili.
•
Watenge kuku wote
walioambukizwa
na
wapewe
antibiotic kama
OTC plus
au salfa.
|
4. Mafua
ya kuku
(Fowl
coryza)
|
Bakteria
|
Kuku
uvimba uso na
macho
Kamasi
hutirirka puani na
mdomoni
Kuhema
kwa shida hata
kukoroma.
Kukohoa.
|
• Usafi
wa banda
•
Kuchanja kuku wote
• Kabla
hawajaambukizwa
kama ni
tatizo sugu
katika
eneo
• Watibu
wanaougua
kwa
kutumia anti biotic
kama
sulphamethazine,
streptomycine
na
vitamin
|
5.
Kuharisha
nyeupe
|
Bakteria
|
Kuharisha
nyeupe na
hamu ya
kula kupungua.
Wadudu
washambuliao
Kuku
|
• Usafi
wa vyombo na
banda
kwa ujumla
•
Watenge kuku
wagonjwa
• Tumia
dawa kama
Furazolidone
au
Sulfadimidine
• Hata
vitunguusaumu menya robo
kilo
utwange nu
kuchanganya
na
maji
lita moja. Chuja
uwapatie
maji haya kwa
muda wa
wiki moja.
|
Wadudu
washambuliao Kuku
|
|||
Viroboto,Chawa,
Papasi
|
|
Kuku
hawatulii, hujikuna
mara kwa
mara.
Hupungukiwa
na damu na
uzito
Wadudu
huonekana
mwilini
|
Wadudu
washambuliao
Kuku
Usafi wa
banda na
mazingira
Banda
lipitishe hewa ya
kutosha
ili liwe kavu
Nyunyizia
kuku na banda
zima
dawa za kuua wadudu
kama
vile Akheri powder,
Malathion,
Servin n.k
|
Kutoa chanjo ya kideri kwa njia ya kuweka matone ya dawa katika macho |
Njia kuu za ujumla za kudhibiti magonjwa ni:
- Kutunza hali ya usafi ndani ya banda na kudhiditi kusiwe na unyevu
- Matandazo yakichafuka yabadilishwe.
- Vyombo vya maji visafishwe kila siku
- Jitahidi uepuke kufuga kwa njia ya huria ili kuku wako wasiambukizwe magonjwa kirahisi
- Epuka kufuga kuku wako pamoja na bata na khanga.Hawa ni wabebaji wa vimelea vya magonjwa ya kuku japo wao hubaki
salama. - Zingatia ratiba za chanjo kwa magonja yasiyo na tiba kama kideri na mengineyo ya virusi
Source: RLDC
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni