191. Jitahidi
kuwa mtu uliye wazi. Uwe mwaminifu binafsi na hata watu wengine wakuamini.
192. Nguvu ya
kutaka kwako itaongezeka sana kama ukidhibiti maneno yako. Mtu anafungwa na
kitu fulani kizuri, huingia katika ugumu sana na kukosa furaha ikiwa kitu hicho
kitatoweka. Watu wenye furaha wakati wote ni wale ambao hufurahia jambo lolote
pasipo kukubali kufungwa na jambo hilo. Ishi maisha rahisi, ya utaratibu, na
kujibidiisha katika uzalishaji. Katika kurahisisha maisha nyakati hizi waza
kuuza runinga yako, acha kufuatilia meseji zisizo na tija, uwe na matumizi ya
wastani, waza kuuza gari yako, jifunze kutulia na kutafakari kila asubuhi na
ondoa mlio katika simu yako unaoweza kukutoa katika kutafakari.
193. Kama
hujacheka katika siku ya leo; fahamu leo hujaishi. Cheka sana na kwa nguvu kama
William James alivyosema, "we don't laugh because we are happy, we are
happy because we laugh." Akimaanisha “hatucheki kwasababu tunayo furaha,
tuna furaha kwakuwa tunacheka”.
194. Soma kitabu
kiitwacho, “The Charisma Factor” Namna
gani unaweza kuendeleza uwezo wa kiasili katika uongozi kama kilivyotolewa na
Robert J, Richardson na S. Katherine Thayer. Ni kitabu kizuri sana kwa kila
anayetaka kuwa kiongozi bora au tayari ni kiongozi na unataka kupiga hatua
zaidi katika uongozi wako.
195. Safiri
mara kwa mara. Kwani kutembelea katika eneo jipya ambalo hujawahi tembelea ni
jambo la msingi sana na inakuruhusu kutambua na kubainisha fursa ambazo
vinginevyo usingezipata.
Kwa
leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram
(+255 625 843 804)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni