196. Kila
mwezi jiwekee malengo katika kuimarisha afya yako. Mfano unaweza kuanza na
mazoezi ya uogeleji au vinginevyo. Lengo likiwa ni kufikia pale ulipokusudia
katika mwezi, andika hilo kwa kumbukumbu na uwaze kufanya tena na tena.
197. Mara
zote vitu huumbwa kwa namna mbili. Upo uumbaji unaoanzia kwenye akili na
uumbaji wa kiuhalisia yaani unaweza kuona na kugusa. Kama ilivyo mipango ya
nyumbani kwamba kwanza utaanza kuiweka katika maandishi kabla ya utekelezaji.
Vivyo hivyo na mipango yako ya siku inapaswa kuanza kabla ya machweo. Fikiria
maajabu ambayo unapenda yawe sehemu katika maisha yako na utashangaa inakuwa
hivyo kadiri unavyosonga mbele. Hii ni sawa kabisa kiuasili.
198. Nenda
kazini na tambua uzuri na ajabu katika mazingira ya asili..
199. Lala
kidogo, matumizi yako yawe ya chini, fanya kazi kwa bidii, utaishi muda mrefu
na kuwa mtu mashuhuri.
200.
Mwisho endelea kusoma mfululizo huu tena na tena na kuwashirikisha wengine!
Mpendwa msomaji na
mfuatiliaji wa makala za "ujasiriamaliafya" tunapenda kukupongeza kwa
ufuatiliaji ulio makini katika kipindi chote ambacho tumekuwa tukitoa makala
hizi na hatimaye leo tunahitimisha. Hata hivyo muhimu kufahamu hapa ni kwamba kazi
iliyokuwa inafanywa ilikuwa ni kuujenga msingi ambao utatumika sasa katika
makala zifuatazo kujenga nyumba. Bila shaka ukifuatana nasi hali yako ya
kutokufanikiwa na kukwama kwama itabadilika kabisa ikiwa tutauzingatia msingi
huu ulio katika mfululizo wa siri 200 za kufanikiwa katika maisha. Hivyo
tujitahidi kuyatendea kazi.
Nahitimisha siku
hii ya leo kwa kukutakia ujenzi mwema na endelea kufurahia
"ujasiriamaliafya" kwa vitu moto moto mbalimbali vitakavyoendelea
kuwekwa kwenye ukurasa wetu huu.
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram
(+255 625 843 804)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni