186. Jaribu kula
matunda na maziwa tuu kwa siku nzima. Watu wa mashariki ya mbali wamemudu
kuimarisha afya zao kupitia mbinu ya kufunga au kuacha kula vyakula vigumu na
kula vyakula laini. Kwa kufanya hivyo baada ya wiki kadhaa utagundua kuimarika
kwa nguvu za mwili wako tofauti na awali na wepesi katika kutembea. Chakula kizuri
kinahitaji kuwa na virutubisho ambavyo utahakikisha vinachanganywa wakati wa
maandalizi ili kuimarisha afya yako.
187. Thamini
furaha ya mshirika wako na kumjengea picha kwamba unathamini kazi yake kila
siku.
188. Ikiwa
una mwenzi, jitahidi kuzitunza kumbukumbu za kuoana kwenu wakati wote.
189. Akili
ni kama bustani, ukipanda basi utavuna. Unapojiendeleza na kuijali akili yako,
itastawi kwa kiwango usichotarajia. Bali ukiacha magugu yaitawale akili yako
kamwe hutafikia malengo yako. Chochote unachokiingiza kwenye akili yako ndicho
kitakachotoka katika akili yako. Kwahiyo epuka kuangalia sinema, vitabu vya
simulizi mbaya, na vitu vyote visivyofaa au vyenye mtizamo hasi. Watu mashuhuri
katika mafanikio ni watu waliochagua kwa umakini vitu vya kuingiza katika akili
zao kabla. Kwa hakika huwezi kupata faraja kutokana na fikra hasi.
190. Tabia
ya kukaa na kusimama kwa siku mara nyingi zaidi ni nzuri katika kuimarisha
misuli yako itakayokufanya mwisho wa siku uifurahie afya yako na kuwa na
uhakika nayo. Hii pia inatengeneza maumbile yako na kukuongezea kujiamini
zaidi.
Kwa
leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram
(+255 625 843 804)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni