181. Angalia
kielelezo cha tabia ya kiwango cha juu kabisa:
•
Umakini
na uhakika katika mawazo na maelezo.
•
Mwenendo
wa kuyachuja mambo na upole.
•
Uwezo
na tabia ya kuyapima mambo kabla ya kuyatendea kazi.
•
Uwezo
wa kujiendeleza mwenyewe pasipo kutegemea mtu fulani.
•
Uwezo
wa kufikia malengo uliyojipangia na ndoto za maisha yako.
182. Maisha
si ujana ni akili. Watu wanazeeka kutokana na mawazo wanayo kuwa nayo
na mawazo hayo huwatoa kabisa katika hali ya ujana. Miaka inafanya ngozi
ijikunje, lakini ukiwa unaiwazia sana inafanya moyo ukunjamane pia. Utazeeka
kulingana na mawazo na wasiwasi ulionao, woga wako, msongo wa mawazo na uzembe.
Njia ya kutunza ujana wako ni kujiamini na kuwa na uhakika ya kwamba wewe ni
kijana wakati wote. Tumaini lako liwe ni ujana.
183. Chunguza
dawa za kichina na zile za kutoka mashariki kama zitakufaa kwa kuweka mwili
wako tatika afya bora na ni vema kushauriana na matabibu ili upate ushauri
stahiki kabla ya kuanza kutumia kulingana na matatizo uliyo nayo ya kiafya.
184. Tumia muda wako vizuri katika vipaumbele vyako
kila siku kwa kufanya kwanza mambo ya msingi katika maisha yako.Ni rahisi
kusema hapana wakati ndiyo inaonekana kutawala ndani mwako.
185. Usiwe
na haraka katika maisha. Katika miaka tuliyonayo tunatakiwa kuendesha maisha
yetu kwa utulivu. Zingatia kile ambacho
ni muhimu na ufanye shughuli ambazo
hazitakufanya uwe na haraka na ambazo zitarudishia uasili wako na zitakufanya uwe na amani. Kaa
kwenye majani na angalia anga kwa muda wa nusu saa na hili siyo rahisi kama
watu wanavyofikiri. Ushauri wangu ni kukufanya upate muda wa mapumziko kwa muda
mfupi ukifurahia utulivu.
Kwa
leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram
(+255 625 843 804)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni