Jumatano, 23 Novemba 2016

NA.171 - NA.175: KUFANYA JAMBO KWAAJILI YA WENGINE.



171. Kumbuka kununua mfuko wa mpango ambao utahakikisha kuwa una chombo kizuri cha kuratibu, kutunza mipango yako na majukumu uliyonayo katika maisha yako kwa utaratibu mzuri.
172. Jisomee vitabu mbalimbali kila baada ya miezi michache ukitafuta hazina katika ujenzi wa tabia kupitia waandishi wa vitabu hivyo. Utajifunza namna ya kuzungumza mbele ya watu wengi kwa usahihi, utabadilika kitabia na kuwa na tabia njema sana, matumizi mabaya ya muda utayaacha, utakuwa na afya nzuri na vitu vingine vingi sana utajifunza kwa gharama ndogo. Utagundua miongoni mwa vitabu hivyo vya zamani ni vizuri sana katika kujenga tabia na nidhamu ya katika maisha.
173. Soma kitabu kiitwacho “The Magic of Believing” kilichoandikwa na Claude M.Bristol. Kitakufundisha namna ya kukabili nguvu ambazo mara kwa mara zilikuwa zikikufuatilia lakini hazikuwa na faida kwako.
174. Tamani kujulikana kama mtu mtulivu, mwenye moyo mzuri na tabia njema. Uwepo wako hapa duniani utakumbukwa kwa muda mrefu hata baada ya kuondoka kwako.
175. Inaaminika kwamba kufanya jambo kwa ajili ya wengine ni imani ya juu sana. Katika wiki moja kuna masaa168 tunayoyatumia, tumia masaa machache kuwahudumia wengine. Wengi wanaamini ukiacha ubinafsi na kuwahudumia wengine baada ya muda mfupi utashangaa inakuwa ni sehemu katika maisha yako. Tumia muda wako kwa wazee wasiojiweza au kwa watoto yatima. Fundisha jinsi ya kusoma au namna ya kuzungumza mbele ya watu wengi na kwa matendo hayo utakuwa umewaachia urithi mzuri sana.

Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: