Jumanne, 22 Novemba 2016

NA.166 - NA.170: NGUVU KATIKA KUTAFAKARI.



166. Kutumia muda katika kufanya maendeleo yako binafsi ni kitu cha msingi sana, usijaribu hata kidogo kupoteza mda wako kwa  kufanya mambo yasiyo muhimu. Kuchukua saa moja kwa masaa ya asubuhi kuangalia watoto wadogo wanaocheza karibu au kutembea polepole ukiwa unaenda mahali fulani ni kupoteza muda. Lakini kwa kutumia muda wako vizuri itakusaidia sana kufanya shughuli zako za uzalishaji binafsi vizuri na hivyo kujiletea maendeleo. Huwezi kufanya vizuri kama hujisikii vizuri.Ukiwa na utulivu mzuri waweza fanya vizuri sana shughuli zako za uzalishaji, pia waweza kuwa mbunifu na kuwa mtu unayeendana na mazingira.
167. Soma kwa bidii, jifunze kwa bidii, cheka sana na uwe na upendo zaidi. Hii itakusaidia kuwa na uchangamfu katika moyo wako.
168. Chagua aina tano za mahusiano ambayo unapenda yatakayo kufanya upande ngazi baada ya miezi sita ijayo. Andika majina ya hao watu ambao unataka kuimarisha mahusiano nao na kila jina moja andika maelezo kwa nini unapenda kuimarisha mahusiano, namna ya kuimarisha mahusiano na kwa muda gani? Huu ni uwanja wa pekee wa kupanga malengo yako. Ni zoezi ambalo litakuletea majibu mazuri sana katika kila uwanja wa kutafuta mafanikio yako. Jiandae kuwa mzazi bora, rafiki mzuri na raia bora. Kuwa mbunifu katika hatua unazochukua kuonesha kwamba umekubaliana nao na unawaheshimu wapendwa wako. Kuwapa taarifa ni vizuri lakini kumbuka utofauti na vipimo vya mawazo yao na umbali kutoka mahali walipo mpaka sehemu ambayo mnakwenda kukaa pamoja na kufurahia.
169. Kumbuka nguvu ya maombi juu. Maombi ni silaha kubwa kuliko silaha zote tuzijuazo duniani katika kutupatia mema tunayoyahitaji.
170. Uwekezaji mzuri katika ukuaji wako binafsi unapatikana kutoka kwenye mafundisho ya kaseti sita ya Reverend Dr.Norman Vincent Peale yaitwayo "The Power of Positive Thinking”. Pata nakala hizo na sikiliza tena na tena. Ndani yake kuna mikakati na mbinu ambazo zitakufanya usiwe mtu wa kushindwa, bali zitakufanya shughuli zako ziishi muda mrefu, ukiwa ni mwenye furaha, na maisha ya kustawi.
 
Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: