Ijumaa, 18 Novemba 2016

NA.161 - NA.165: UJASIRI, HESHIMA NA UADILIFU.



161.  Kila siku fanya vitu viwili ambavyo ulikuwa hupendi kuvifanya. Hii itakuwa ni maandalizi ya taarifa ambayo umekuwa ukiiweka pembeni. Usiangalie ni jambo dogo kiasi gani wewe fanya tuu! Baada ya muda mfupi utaanza kuona shughuli hizo zilizokuwa zinaonekana hafifu kwako si hafifu tena, na bidii yako binafsi itaongezeka na matokeo yako yataongezeka. Jaribu kufanya hivyo kwani hii ni mbinu ya zamani ambayo ilitumika na watu mbalimbali katika kujenga nguvu ya tabia.
162. Furaha ya kweli hutokana na kitu kimoja: mafanikio ya malengo, iwe ya binafsi, kitaalamu au vyovyote. Unakuwa na furaha pale unapohisi unaongezeka. Pale unapohisi kwamba mchango wako unakupeleka katika ndoto zako, utajihisi kuwa na nguvu zisizo kifani na shauku kubwa. Kuutumia muda katika jambo ambalo malipo yake ni kidogo kutokana na kuacha kujisikia katika kujifurahisha mfano kuangalia Runinga ni muda unaoupoteza na hauwezi kuupata tena. Kujifurahisha ni muhimu lakini tafuta namna ya kuufidia muda huo na shughuli za uzalishaji ambazo zitakupelekea kufikia malengo yako ya mafanikio. Furaha huja kwa kutenda na si kulala.
163. Huko Ufaransa, Napoleon wa Tatu alikuwa na uwezo wa kukumbuka majina ya watu wote aliokutana nao. Siri kubwa ilikuwa ni kusema “samahani sana, nikumbushe majina yako” kila alipokutana na mtu ambaye hajawahi kutana naye. Hii inafanya jina kujirudia rudia na kulazimisha kukaa katika kumbukumbu. Na kama jina lilikuwa gumu, aliomba litamkwe kwa alfabeti kikamilifu.
164. Msingi wa wa-China umejengwa juu ya falsafa hii katika maisha takribani miaka maelfu sasa: kujijenga katika roho ya ujasiri, heshima na uadilifu. Kadiri unavyo rudia rudia kujiweka katika hali hiyo ndivyo unavyokuwa mtu wa kipekee unayeheshimika na wengi. Tumia bidii yako kuona kwamba wewe nawe unapata sifa hiyo.
165. Mbinu pekee ya kukabili fikra kinzani zinapokuja kwako kwa nia ya kukukatisha tamaa na kukuzuia kuyaendea mafanikio ni kuwa na nyenzo ya kuyazuia mawazo na akili. Mawazo ya kushindwa yanapoingia kwako kwanza hunabudi kujitambua na kutamani kuyaondoa kwa kutumia fikra za kushinda mara moja. Unaweza kutamka kinyume chake kwani mawazo na akili husikia unapotamka mfano “mimi ni jasiri” au “mimi naweza” kadiri unavyotumia ulimi wako vizuri dhidi ya fikra hasi ndivyo fikra hasi zitakavyotoweka na fikra chanya zitatawala ndani mwako.
Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: