Jumatano, 16 Novemba 2016

NA.156 - NA.160: ACHA MADIRISHA YA AKILI YAKO WAZI.



156. Hakikisha kazini kwako unajulikane kama mtu mbunifu. Kaa chini na andika mawazo kumi kwenda kwa kiongozi wako ambayo utajadiliana naye juu ya kuboresha kazi zako na ubora wa eneo lenu la kazi kwaujumla. Jiweke katika hali itakayo kutambulisha kuwa mtu mwenye mawazo yanayobainisha changamoto na namna ya kuzishughulikia kwa umakini na shauku kubwa.
157. Moyo uliochangamka ni dawa nzuri! Hivyo jifunze kucheka peke yako.
158. Madirisha ya akili yako yaache wazi wakati wote na kujiweka tayari kupokea mawazo tofauti tofauti ambayo ni kama fursa kwako kuchagua ufanye lipi na uache lipi.
159. Jaribu kwenda siku moja nzima bila kusema nitafanya bali lenga kupokea toka kwa wengine. Sikiliza toka kwa wengine na kwa hakika utajifunza vitu vingi vipya na vya ajabu sana na zaidi kujiongezea marafiki.
160. Tumia saa moja katika siku kwa ukimya kabisa isipokuwa kujibu maswali mojakwa moja. Hata hivyo jibu swali utakalo ulizwa moja kwa moja bila kutaka kuendeleza mazungumzo. Ni kawaida ya binadamu kuzungumza kitu kwa kurudia rudia.  Kama wahenga wa mashariki wafanyavyo si tu itakujengea nguvu ya kuhiari bali itakujengea kueleweka kwa wepesi na lugha ya inayoonesha umakini ambayo ni muhimu kwa mawasiliano ya uhakika.
Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: