Jumanne, 15 Novemba 2016

NA.151 - NA.155: FIKIRIA WEWE NI CHUNGWA.



151. Kila aliyefanikiwa na kupata matokeo makubwa juu ya jambo analolifanya, kwanza alijijengea matumaini makubwa ndani yake kabla ya kufikia hatua hiyo. Pasipo matumaini mwelekeo wa maisha hupotea na ugumu hutokea katika kila hatua unayopiga. Matumaini ni tabia ya muhimu katika maisha.
152. Hebu leo orodhesha tabia saba nzuri unazotamani zingekuwa katika maisha yako alafu zibandike karibu kabisa na kitanda chako. Alafu kila asubuhi lenga kwenye tabia moja tuu ambayo utahakikisha katika siku yako unaitekeleza. Baada ya wiki moja utagundua mabadiliko kidogo katika maisha yako. Ndani ya mwezi mmoja utabaini kuyafanya vizuri yote. Ndani ya miezi miwili tabia zote saba zitakuwa zako.
153. Unazo sifa nyingi kadiri unavyofanya mambo yako na watu wengi tofauti tofauti kwani kila mmoja hukufikiria tofauti kabisa. Kitu cha msingi hapa kuangalia na kujali ni tabia yako mwenyewe halisi. Unaouwezo kamili wa kumiliki au kuisimamia tabia yako, jichunguze na kujijengea tabia njema. Kama tabia yako ni njema na unasimamia hilo. Kila mwenye mtizamo chanya juu yako atapenda kukufuata au kwenda na wewe.
154. Chukulia wewe ni chungwa. Kile kilicho halisi ndani yako ndicho kitakutoka. Kama akili yako imejaa mawazo ya utulivu, mtizamo chanya, nguvu, ujasiri na huruma, kama mtu akija kwako hiyo ndiyo juisi itakayo kutoka ndani yako.
155. Maisha yetu hayaelezewi katika umilele jinsi itakavyokuwa. Tupo lakini ni kama katika hatua ndogo sana katika sayari hii. Kama ijulikanavyo hatutachukua chochote tunapoyaendea maisha hayo ya milele, basi maana halisi ya uwepo wetu hapa ni kutoa na kuhudumia wengine. Jitahidi kuwa hivyo wakati wote. Unapoamka asubuhi na mapema tamka maneno haya ya kujitega mwenyewe: “leo nitahudumia wengine, nitawajali watu leo na nitakuwa mwema pia”. Aina hii ya maisha itakulipa malipo mengi kama ukidumu katika kusudi la kuwasaidia wengine badala ya kuwaza kujinufaisha wewe mwenyewe binafsi.
Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: