Jumapili, 13 Novemba 2016

NA.146 - NA.150: BILA HII KILA MTU ATAKUONA HAUFAI.



146. Jenga tabia ya kufanya shughuli sahihi kwa wakati sahihi na mahali sahihi, hii itakusaidia kuwa na mafanikio makubwa.pia hii itakufanya kuwa na nidhamu kwa wenzio na kuonesha unawajali sana. Bila hii kila mtu atakuona hufai. Usiwahi sana na usichelewe sana, pangilia muda wako na uwepo eneo la tukio mapema kama mlivyokubaliana na wenzio ili uwe na utulivu. Kwa kufanya hivyo tabia iliyo adimu kwa wengi utakubalika na kila mtu popote utakapoenda na kukaribishwa vizuri na kupendwa sana.

147. Simu ipo kwa ajili ya kurahisisha mawasiliano yako sio kwa ajili ya wengine wanaotaka kuwasiliana wewe.Kama umetingwa sana na kazi usijibu simu yoyote ambayo umepigiwa subiri muda utakao kuwa huna kazi na umetulia kabisa ndipo uwasiliane na huyo mtu.Usiruhusu muingiliano wa mawazo wakati wa kazi, utapoteza muda.Mara nyingi simu zinazopigwa huwa hazina mambo ya msingi ya kuzungumzia na hupoteza muda mwingi sana kwa kuongea. Watu wengi wamekosa mafanikio na kupoteza muda wao kwa kutumia muda mwingi kuongea na simu badala ya kufanya kazi zitakazo waongezea kipato.
148. Uianze siku yako vizuri. Kabla ya kukiacha kitanda chako kila asubuhi, mshukuru Mungu kwa kukuamsha salama wewe na familia yako, pia mwambie asante kwa kuiona siku mpya na kwa kila kitu kizuri alichokupa wewe na familia yako. Anza kuiona hiyo siku ni nzuri sana kwako na itakuwa ya   furaha, mafanikio na utulivu kwako. Na kama unaamini hayo hakika ndivyo yatakavyokuwa. Siri ya matumizi mazuri ya muda wako ni kuona kila siku kama ni nafasi ya kipekee na haitakuja tena
149. Jitahidi kumshirikisha mambo yako mwenzi wako. Kwa kufanya hivyo mahusiano yenu yataimarishwa na kuwafanya mwende kwa kasi ya pamoja. Kushirikishana vitu vya msingi au changamoto ni jambo ambalo huimarisha sana mahusiano na kuthaminiana sana.
150. Kila siku jisurutishe kufanya vitu vinavyoonekana ni vigumu na jitahidi kufanya zaidi ya kawaida. Katika uwanja wa mashindano washindi hujitahidi kusukuma bahasha zao za mafanikio kuelekea kileleni kwa kila wapatapo nafasi. Fanya vitu vile unavyoogopa kuvifanya kwamba haviwezekani na ndivyo kifo cha uoga ndani mwako kitakavyokuja. Washindi mara zote hufanya vitu vile ambavyo watu wengi wenye maendeleo ya chini huwa hawafurahii kufanya. Hivi ndivyo tabia na shauku vinaimarishwa ndani ya mtu. Shughulika na udhaifu ulio ndani mwako. Anza kufanya vile vitu ambavyo ulivitenga na kutokuvifanya. Andika vile vitu katika orodha ambavyo umevibeza mara nyingi. Fanyisha mazoezi misuli yako ya nidhamu utakutana na siku ambayo utajisikia kujaribu kufanya vitu vile ambavyo kwa kawaida usingevifanya ndivyo mabadiliko yatakavyokuja kwako.
Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: