Alhamisi, 10 Novemba 2016

ELIMU YA MADINI JOTO



UTANGULIZI
Ø  Upungufu wa madini joto ni tatizo kubwa linaloathiri afya na maendeleo ya jamii ikiwa ni pamoja na uzalishaji mali na uchumi.
Ø  Tatizo la upungufu wa madini joto hapa Tanzania ni la tatu kwa ukubwa katika matatizo ya lishe, likitanguliwa na tatizo la upungufu wa nishati na utomwili na upungufu wa wekundu wa damu.
Ø  Ukubwa wa tatizo la upungufu wa madini joto huanishwa kwa kupima uvimbe wa tezi la shingo na matumizi ya chumvi yenye madini joto.
Ø  Tafiti za 2004 zinaonyesha kuwa uvimbe wa tezi la shingo ni  7% huku,
Ø  Utafiti wa 2010 ukionyesha kuwa kaya zinazotumia chumvi yenye madini joto ni 82% na;
Ø  Asilimia 47 ya kaya zinatumia chumvi yenye kiwango cha madini joto ya kutosha. 

Mada ya 1:
TATIZO LA UPUNGUFU WA MADINI JOTO MWILINI
MALENGO YA ELIMU YA MADINI JOTO
Mwishoni msomaji utaweza:
Ø  Kufahamu maana na umuhimu wa madini joto
Ø  Kuelezea ukubwa wa tatizo hapa Tanzania na kutaja maeneo yanayoathiriwa zaidi na upungufu wa madini joto
Ø  Kuelezea sababu zinazochangia upungufu wa madini joto mwilini
Ø  Kuelezea madhara na athari zitokanazo na upungufu wa madini joto mwilini

Umuhimu wa madini joto
Ø  Madini joto ni moja ya virutubishi muhimu kwa ukuaji mzuri wa akili na mwili.
Ø  Madini hayo hupatikana ardhini.
Ø  Binadamu anahitaji madini joto kiasi cha kijiko kimoja tu cha chai kwa maisha yake yote.
Ø  Kwa wastani mtu mzima anahitaji kiasi cha mikrogramu 100-150 ya  chumvi yenye madini joto kila siku.
Ø  Mahitaji kwa akina mama wajawazito ni makubwa zaidi (mikrogramu 175). 
Ø  Ingawa kiasi hicho cha matumizi ya madini joto ni kidogo sana lakini umuhimu wake mwilini ni mkubwa sana.
Ø   Ili kukidhi mahitaji ya mwili, binadamu anatakiwa apate madini joto kila siku. Kwa maana hiyo madini joto lazima yawe sehemu ya chakula chake.
Ø  Madini joto hutumika katika kutengeneza vichocheo au homoni za tezi la shingo “thyroid hormones”.
Ø  Homoni hizi husaidia katika ukuaji bora wa mwili na ubongo pamoja na mfumo mzima wa fahamu.
Ø  Iwapo madini joto yatakosekana, kichocheo hiki kitashindwa kutengenezwa na hatimaye mtu atapata madhara. 
Ø  Madini joto pia ni muhimu wakati wa ujauzito kwa ajili ya ukuaji wa mtoto aliye tumboni, kuzuia ulemavu wa akili na mwili na ukuaji mzuri wa mtoto baada ya kuzaliwa.
Ø  Madini joto huhitajika kwa wingi wakati wa mabadiliko ya kimwili kama vile wakati wa kuvunja ungo au kubarehe.
Ø  Madini  ni muhimu katika kuongeza  uwezo wa kuelewa,kutenda na  kufundishika.
Ø  Kwa watu wazima madini joto huongeza uchangamfu wa mwili hivyo kuongeza uwezo wa kufanya kazi na kuongeza tija.

UKUBWA WA TATIZO
Ø  Tanzania ni kati ya nchi ambazo zinaathirika kwa kiwango kikubwa na tatizo la upungufu wa madini joto mwilini.
Ø  Tatizo hili linawaathiri watu wengi na hasa wanaoishi sehemu za miinuko  za nyanda za juu kusini, yaani mikoa ya Njombe, Mbeya, Iringa na Rukwa.
Ø  Mikoa mingine inayoathirika  ni Ruvuma, Kigoma, Kagera na baadhi ya sehemu za mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Dodoma na Morogoro. 
Ø  Matumizi ya chumvi yenye madini joto katika kaya yamekuwa yakiongezeka hadi kufikia 83% na yanatarajiwa kupunguza kwa kiasi kikubwa au kutokemeza  kabisa tatizo la upungufu wa madini joto mwilini.

SABABU ZA UPUNGUFU WA MADINI JOTO MWILINI
Ø  Madini joto hupatikana ardhini. Binadamu huyapata madini hayo kwa kula vyakula vinavyopatikana kwenye ardhi hiyo.
Ø  Kiasi cha madini joto katika chakula hutegemea wingi wa madini hayo ardhini.
Ø  Maeneo ya miinuko na milima huwa na kiasi kidogo cha madini hayo.
Ø  Hii ni kwa sababu katika maeneo hayo madini joto yanakuwa yamepotea kutokana na kuchukuliwa na maji (mvua, miti, chemchem, mafuriko) na kuelekezwa mabondeni na baharini/ziwani.
Ø  Kwa sababu hii vyakula vya baharini au vinavyopatikana mabondeni huwa na madini joto kwa kiasi kikubwa sana.
Ø  Wakati huohuo watu waishio maeneo yenye miinuko na milima hupata  upungufu wa madini joto.

ATHARI ZITOKANAZO NA UPUNGUFU WA MADINI JOTO MWILINI
Ø  Mtu anapokosa madini joto ya kutosha mwilini hushindwa kutengeneza homoni za tezi la shingo,  upungufu huu una athari kubwa za kiafya.
Ø  Mifumo ya mwili iliyo mingi huathirika kwa viwango mbalimbali lakini ubongo wa mtoto aliye tumboni huathirika zaidi. 
WAKATI WA UJAUZITO:
  • Mimba kuharibika
  • Mtoto kuzaliwa akiwa mfu (amekufa)
  • Mtoto kuzaliwa kabla ya wakati wake (njiti)
  • Mtoto kuzaliwa na uzito pungufu
  • Mtoto kufa akiwa mchanga
  • Mtoto kuzaliwa na ulemavu wa viungo
  • Mtoto kuzaliwa akiwa kiziwi na kuishia kuwa bubu 
  • Kudumaa kwa mwili na utaahira
       Cretinism
Ø  Hii ni hali inayojitokeza panapokuwa na upungufu wa madini joto uliokithiri ambao hutokea tangu mtoto akiwa tumboni kama inavyoonyesha katika kielelezo cha picha ya kwanza.
Ø  Mara nyingi mtoto huzaliwa na mtindio wa ubongo.  Pamoja na hayo mtoto huweza kuwa kiziwi au bubu  kudumaa kwa akili na mwili.

WAKATI WA UTOTO
Ø  Kuchelewa katika hatua za ukuaji na maendeleo
Ø  Ugumu katika kuelewa, kutenda na kufundishika
Ø  Kuchelewa kubarehe au kuvunja ungo
            Wakati wa Utu Uzima
Ø  Endapo patakuwa na upungufu au kukosekana kwa madini joto, tezi hilo litachochewa kufanya kazi ya ziada ya kutengeneza kichocheo hicho hatimaye kuongezeka ukubwa.
Ø  Kuvimba kwa tezi la shingo  " Goitre 
Ø  Uvimbe wa tezi la shingo unaweza kuwa mkubwa kiasi cha kubana njia ya chakula na kufanya mtu kupaliwa au kumeza chakula kwa shida. Uvimbe pia unaweza kubana njia ya hewa na kusababisha kupumua kwa shida.
Ø  Kupungua kwa kasi ya kufikiri na kutenda(kufanya) kazi
Ø  Kutostahimili hali ya baridi
Ø  Kuwa na hali ya ulegevu, kukosa uchangamfu
Ø  Hali ya kufunga choo
KIJAMII NA KIUCHUMI
Ø  Jamii hutumia muda mwingi na rasilimali katika kuwatunza waathirika wa upungufu wa madini joto.
Ø  Mifugo pia huathirika na upungufu wa madini joto, kama walivyo binadamu;
Ø  kuharibu mimba, kudumaa na kuongezeka kwa vifo. Yote hayo husababisha hasara za kiuchumi.
Ø  Madini joto ni moja ya virutubishi muhimu kwa ukuaji mzuri wa akili na mwili .
Ø   Madini haya hupatikana ardhini.
Ø  Mahitaji ya madini joto kwa binadamu ni kiasi cha ug. 100-150 kwa siku.
Ø  Mvua za mara kwa mara huyachukua madini joto kutoka ardhini katika sehemu za miinuko kwenda mabondeni, baharini /ziwani na kusababisha vyakula vinavyolimwa katika maeneo hayo kuwa na upungufu wa madini joto
Ø  Madhara na athari za upungufu wa madini joto ni pamoja na kuvimba kwa tezi la shingo, udumavu wa akili na mwili, matatizo ya uzazi, vifo vya watoto na kushuka kwa hali ya uchumi na maisha.
Mada ya 2
Mikakati ya Kukabiliana na Upungufu wa Madini Joto
Ø  Kumekuwa na mikakati kadhaa ya kukabiliana na tatizo hili nchini ambayo imesaidia sana kupunguza tatizo la upungufu wa madini joto katika  maeneo yanayoathiriwa sana na tatizo hili.
Ø  Hapa nchini baadhi ya mbinu zilizotumika ni pamoja na Utoaji wa madini joto ya nyongeza, uwekaji wa madini joto kwenye chumvi, uhamasishaji wa matumizi wa chumvi yenye madini joto na ufuatiliaji wake katika jamii.
 Utoaji wa Madini joto ya nyongeza km:
    • Lugol’s iodine (matone ya vitamin A)
    • Dawa ya sindano yenye madini joto
    • Vidonge vyenye madini joto
        Uchanganyaji wa Madini joto kwenye chumvi
o     Uagizaji wa mashine na vifaa vya kuchanganya chumvi na madini joto km; madini joto, iodine test kits na vifungashio
o     Mafunzo kuhusu matatizo yatokanayo na upungufu wa madini joto pamoja na uzalishaji wa chumvi bora na yenye madini joto kwa Maafisa Afya na wazalishaji chumvi.
Elimu kwa umma kwa kutumia mkakati wa mawasiliano (Mikutano ya hadhara)
    • Uhamasishaji wa viongozi katika ngazi mbalimbali zikiwemo halmashauri zote.
    • Utumiaji wa vyombo vya habari km TV, Radio, Magazeti nk.
    • Uhamasishaji wa wazalishaji chumvi kujiunga ktk vikundi
    • Kuanzishwa kwa Chama cha Wazalishaji Chumvi Tz na kuwepo kanda tano, Chama kina majukumu yafuatayo:
      • Kuwaunganisha wazalishaji chumvi na wadau wengine
      • Kufuatilia uzalishaji wa chumvi yenye madini joto
      • Kuhakikisha upatikanaji wa madini joto na vifaa vingine
      • Kuhamasisha wazalishaji chumvi kuhusu uzarishaji wa chumvi yenye madini joto
    • Kuwepo kwa Kamati Ya Kitaifa inayoratibu mpango wa kudhibiti upungufu wa madini joto.
    • Kuanzishwa kwa sheria ya chumvi
Ufuatiliaji na tathmini:
      • Katika ngazi ya jamii
      • Kwenye mashamba ya chumvi, maduka na viwandani
      • Utekelezaji wa sheria ya chumvi
MAFANIKIO
  • Ongezeko la kaya zinazotumia chumvi yenye madini joto kutoka 0% (1980) hadi  82% (2010)
  • Idadi kaya zinazotumia chumvi yenye kiwango cha madini joto ya kutosha zimeongezeka kutoka 43% (2004) hadi 47% (2012)
  • Uvimbe wa tezi la shingo umepungua kutoka 25% (1980) hadi 7% (2004)
  • Uwepo wa maabara 18 za kufuatilia ubora wa chumvi yenye madini joto. Kati ya hizo; 6 ni za wazalishaji chumvi (Dsm, Tanga, Bagamoyo,Kilwa, Lindi, Mtwara),12 zipo ktk wilaya zinazozalisha chumvi kwa wingi (Ruvuma, Mbeya, Kyela, Iringa, Dodoma, Morogoro, Arusha, Mwanza, Tabora, Mtwara, Njombe na Tanga)
MIKAKATI ENDELEVU:
  • Kuhakikisha upatikanaji wa madini joto kwa wazalishaji chumvi
  • Kuimarisha ufuatiliaji wa chumvi yenye madini joto;
  • Kuimarisha utekelezaji wa sheria ya chumvi;
  • Kuhamasisha umma kuhusu matatizo yatokanayo na upungufu wa madini joto mwilini
  • Kuwawezesha wazalishaji wadogo wa chumvi ktk yafuatayo:
Ø  Upatikanaji wa madini joto wakati wote.
Ø  Kuwapatia mafunzo ya uzalishaji bora wa chumvi yenye madini joto.
Ø  Kuhakikisha upatikanaji wa  test kits na vifaa vingine muhimu km vile vya maabara na pampu.
Ø  Kuoanisha ufuatilaji wa chumvi yenye madini joto na programu nyingine:
Ø  Juhudi zimefanyika katika kuingiza masuala ya kudhibiti upungufu wa madini joto na ufuatiliaji wa chumvi yenye madini joto katika mipango ya halmashauri badala ya kutegemea wafadhili.
Kuhamasisha viongozi:
Ø  Katika ngazi za maamuzi juu ya matatizo ya upungufu wa madini joto mwilini na uzalishaji wa chumvi yenye madini joto.
Ø  Katika ngazi za halmashauri ili waweze kuingiza masuala ya kudhibiti upungufu wa madini joto na ufuatiliaji wa chumvi yenye madini joto katika mipango ya halmashauri
CHANGAMOTO:
Ø  Uwepo wa wazalishaji wadogo wengi wa chumvi waliotawanyika ktk maeneo tofauti na maeneo mengine si rahisi kufikika
Ø  Kutokuwepo na upatikanaji endelevu wa madini joto
Ø  Mapungufu katika mfumo wa usambazaji wa madini joto
Ø  Gharama kubwa ya madini joto (kg 1 = Sh. 60,000/=)
Ø  Usimamizi hafifu wa utekelezaji wa sheria ya chumvi
Ø  Wazalishaji kutofuata vigezo vya uzalishaji bora wa chumvi yenye madini joto (Viwango vya madini joto, usafi, uhifadhi n.k)
Ø  Uelewa mdogo kuhusu:
Ø  Uchanganyaji wa madini joto kwenye chumvi kwa wazalishaji,
Ø  Umuhimu wa matumizi ya chumvi yenye madini joto kwa jamii
MATARAJIO:
  • Kuendelea kuhamasisha viongozi, wazalishaji chumvi na jamii
  • Kuimarisha ufuatiliaji wa chumvi yenye madini joto na utekelezaji wa sheria ya chumvi yenye madini joto
  • Kutafuta njia ya upatikanaji endelevu na usambazi mzuri wa madini joto
  • Kufanya tafiti kwa makundi yenye mahitaji maalum mf. Watoto wadogo, wanawake wajawazito na wazee.
IMEANDALIWA NA;
 Beatrice Bethod-Afisa Lishe-Ludewa
Simu Na-0752472813
Email- beatricebethod@gmail.com

 
 
 

Hakuna maoni: