Alhamisi, 10 Novemba 2016

NA.141 - NA.145: UPO JINSI ULIVYO KWASABABU YA VYAKULA UNAVYOKULA.



141. Watu wengine huviona vitu kama vilivyo na kusema “kwanini?” Ninaota ndoto ya vitu ambavyo sijawahi kuviona na kusema “kwanini iko hivi na si vinginevyo?” Hii ni nukuu toka George Bernard Shaw.
142. Tumia mbinu zifuatazo katika kuongeza ubora wa akili yako katika kutafakari:
1.  Jizoeshe kutafakari kila siku mahali palepale na muda uleule ili ufahamu wako uwe tulivu.
2.  Alfajiri ni muda mzuri na tulivu sana kwa kutafakari. Hili litakuongezea amani katika kuyaendea mafanikio yako.
3.  Kabla ya kuanza amru ufahamu wako utulie kwa kutumia hisia “nitakuwa makini na mtulivu kuanzia sasa”.
4.  Kama mawazo yanakujia usilazimishe kuyaondoa bali yaache yakutengenezee njia nzuri ya mafanikio.Tambua kwamba ufahamu wako ni kama  ziwa lisilo  hata na mawimbi.
5.  Kaa kwa dakika kumi kwa mara ya kwanza baadae ongeza muda kila baada ya dakika kumi. Baada ya mwezi mmoja au miwili hautakuwa unaingiliwa na mawazo yanayo changanya ufahamu wako na utahisi utulivu wa hali ya juu ambao hujawahi kutana nao.
143. Weka urafiki wa haliya juu na watu mahusiano haya ni muhimu na itakusaidia kuwa na afya nzuri na maisha yenye mafanikio.Tafuta muda mchache kila siku wa kuwasiliana na watu ambao hujawasiliana nao kwa muda mrefu. Onesha upo pamoja nao na angalia matokeo baada ya kuwasiliana nao. Jenga tabia ya kuwa na urafiki mzuri na wa muda mrefu na watu. Pia weka kipaumbele kupata marafiki wapya bila kujali utakuwa nao kwa muda gani. Hii ni moja ya njia ya mtu kufurahi ambayo watu wengi huikosa.
144. Ni vizuri kuupata muziki laini baada ya shughuli zako nzito ili kukuburudisha na hakika muziki wa namna hii huiburudisha roho yako.
145. Ishushe hamu uliyonayo kwa kunywa maji mengi. Shusha kiu yako kwa kunywa maji tena na tena ukifikisha glasi kumi kwa siku itakufaa sana! Inauweka vizuri mwili wako. Pia jizoeshe kunywa supu ikiwa na mchanganyiko na vyakula vyenye wanga ili kukuondolea njaa na kuufanya mwili wako ujisikie vizuri. Upo jinsi ulivyo kwasababu ya vyakula unavyokula na hakikisha wakati wote mlo wako unakuongezea nguvu na kuimarisha akili yako.
Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: