Jumanne, 8 Novemba 2016

NA.135 - NA.140: FIKIRI JUU YA VITU VIZURI ULIVYOVIFANYA...



136. Furahi kazini na ujulikane kwa wengine kama mtu wa kufanikiwa.
137. Wazo huleta taswira katika akili. Taswira katika akili huzalisha mazoea ya akili mwishowe katika kupambanua aina ya mambo. Tawala mawazo yako, utawale kumbukumbu zako na utawale maisha yako; ukitawala maisha yako utatawala na mafanikio yako.
138. Tambua nguvu kubwa ya mawazo tofauti. Hii ni kanuni nyepesi inayohusisha badiliko la mtizamo chanya kuwa mtizamo hasi na vizuizi vinavyoingia akilini mwako na kupunguza malengo yako wakati wote. Mfano; Jumapili jioni unaweza kufikiria “natamani nisingeenda kazini kesho baada ya mapumziko na raha niliyoipata mwishoni mwa wiki”.Ghafla utaona yanakuja mawazo yanayo kabili nia hiyo hata kabla haijaanza kujijenga. Mfano mwingine “siwezi kusubiri kwenda kazini kutokana na shughuli zinazosisimua zinazoendelea na hisia ya ajabu kwa matokeo na changamoto nilizopata mwishoni mwa wiki”. Alafu fikiri bahati uliyonayo kwamba una kazi na jinsi unavyoweza kufanya kwa jitihada zako hata kuwa na matokeo makubwa. Fikiria na orodhesha vitu vinavyoweza kukufanya ufanye vizuri vilivyomo ndani mwako na rudia kwa kufanya hivyo tena na tena. Baada ya muda mfupi utaona vitu vile vya kukuvunja moyo na kukukatisha tamaa vikitoweka kimoja baada ya kingine na kukufanya ufanye vizuri zaidi na kuifurahia wiki yako kwa ari zaidi.
139. Jizoeshe kujipima wewe mwenyewe. Ben Franklin aliitaja hii kama mbinu muhimu zaidi katika mafanikio ya mtu binafsi. Tumia dakika kumi kila siku kujichunguza wewe mwenyewe binafsi. Fikiri juu ya vitu vizuri ulivyovifanya katika siku yako na tabia mbaya inayoweza kukurudisha nyuma ambayo unalazimika kuibadili ili uongezeke na kustawi sana! Watu waliofanikiwa ni wale wanaotafakari mambo zaidi ya wengine. Tendo la kujiakisi litakuondolea sifa mbaya na kuunoa ubongo wako. Baada ya muda utashangaa makosa unayofanya ni machache sana na ujasiri juu yako utaongezeka na kukupeleka ngazi nyingine ya juu zaidi.
140.  Hadhari nzuri na ya kufaa imejengwa ndani ya akili yako. Kama huamini jaribu yafuatayo:
1.      Keti katika kiti cha kawaida kwa wastani wa dakika 10 kabla ya kwenda kulala.
2.      Funga macho yako alafu taratibu elekeza mikono yako magotini.
3.      Pumua kwa nguvu kwa dakika chache (vuta hewa kwa sekunde tano, kisha tulia kwa sekunde kumi na pumua kikamilifu)
4.      Rudia yafuatayo mwenyewe angalau mara ishirini: “Nitaamka nitakapojisikia vizuri, mchangamfu na mwenye shauku.” Maneno hayo lazima yatamkwe kwa hisia na shauku. Alafu baada ya sekunde chache hebu tafakari wewe mwenyewe pale unapoamka kwa wakati unaoutaka na fikiri utajisikiaje!!?. Utajikuta unaamka muda uutakao bila hata ya mazoezi.

Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: