131. Kuza
akili ya mshangao juu ya dunia. Uwe mtafiti wa mambo. Tafuta furaha katika vitu
walivyonavyo wengine ambavyo wewe kwasasa huna. Jitahidi kusoma vitabu bora
kabisa ambavyo wazazi wako walivipenda sana. Panga kutoka nje ya mji wako kwa
matembezi ya kawaida wiki linalofuatia na tembelea maeneo yenye utulivu, maeneo
yenye uasili kwa siku chache tu. Jaribu kujirudisha nyuma kidogo na uangalie
yale yaliyopita ukitafakari ya mwilini na ya kiroho pia. Kufanya vyote hivyo
kuna maana sana katika kuyaboresha maisha yako.
132. Watumie
jamaa au marafiki zako kadi za kumbukumbu ya kuzaliwa na andika maneno machache
mara kwa mara kuonesha kwamba unawajali na pia unathamini mahusiano yako na
wao. Sote tuna shughuli nyingi lakini kutumia dakika tano katika wiki
kuwakumbuka marafiki na jamaa zako, kwa mwaka mzima utakuwa umetuma kadi 52. Huu
ni uwekezaji mdogo kama dhamana ya gawio ambalo litakuja kwako au litakufuata.
133. Kumbuka
na tumia jina la mtu unapoongea na watu. Jina la mtu linaleta upekee na
kuongeza uzito kwake.
134. Kutoka
katika mazoea na kufanya jambo ambalo si la mara kwa mara kama kuangalia anga
la bluu, kutembelea maeneo yenye uasili kunakuongezea nguvu zaidi na
kuchangamsha akili yako. Tembelea misitu ya asili na kaa kidogo ukipata upepo
tulivu au waweza kodi mtumbwi na kutalii kidogo maeneo ya bahari au maziwa.
Kufanya hivyo kutakushangaza baada ya kurudi. Kwani utajiona kama mpya kabisa.
135. Kila
baada ya wiki kadhaa acha saa yako nyumbani. Katika jamii tumekuja kujikuta
tunafungwa na saa zetu kiasi cha kuongozwa na saa kwa kila jambo kama msimamizi
wa majukumu yetu. Nenda siku nzima ukifanya yale uliyokusudia kuyafanya kwa
usahihi hata kama ingekuchukua muda mrefu sana. Tumia muda na watu mashuhuri
bila kukimbia kimbia katika miadi mingine. Okoa muda na lenga katika jambo
lililo muhimu badala ya vitu vingine vya dunia ambavyo wakati mwingine
vinaonekana ni vya muhimu zaidi kuliko uhalisia. Acha saa na upate muda ulio
bora.
Kwa leo tuishie hapa na
karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram
(+255 625 843 804)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni