Alhamisi, 3 Novemba 2016

NA.127: .....UUCHEKE USHINDANI MDOGO MDOGO.....



  Ni muhimu kuvunja mazoea yanayojengeka ndani mwako yanayokuletea mashaka katika mafanikio unayotaka kuyafikia na uyafunike mashaka hayo na taswira ya jambo unalotaka kuliendea na pia uucheke ushindani mdogo mdogo unaotokea katika safari yako ya mafanikio. Endelea kujipa moyo juu ya ugumu unaopitia na kusema kwa kurudiarudia kwamba hili ni jambo la muda mfupi tuu! Alafu chukua kipande cha karatasi, andika mashaka uliyonayo ndani mwako.Ugawe muda wako kidogo kuyafikiri hayo, yatenganishe matatizo yako na kubuni njia mbadala ya kuyakabili. Kwa kufanya hivyo mtizamo hasi uliomo ndani mwako na nguvu ya mazoea itapotea kabisa.

Hakuna maoni: