Jumatano, 2 Novemba 2016

NA.121 - NA.126: LEO YAKO NI MWANAFUNZI WA JANA.



121. "Leo yako ni mwanafunzi wa jana." - Benjamin Franklin
122. Kama umechagua njia mbili basi nenda na njia ile inayokupa shauku zaidi. Jiridhishe kwa kukokotoa vihatarishi utakavyo kutana navyo katika kukupa matokeo uliyo ya kusudia.
123. Kila siku jitahidi kupata muda wa kujitenga na kelele, msongamano wa watu na uende mahali penye utulivu na amani kwa nia ya kujipima au kujichunguza, usomaji wa kuzama au mapumziko ya kawaida.
124. Angalia, mtu yeyote aliyetembea duniani amefanikiwa! Unaweza kufanikiwa katika mtizamo sahihi, uvumilivu na bidii ya kazi. Mawazo na akili dhaifu havinabudi kudhibitiwa na kukomeshwa. Malengo ya mtu lazima yatulie kuuangalia mwisho wa jambo lenyewe na hilo ndilo jambo la muhimu.
125. Jijengee mazoea ya kujikumbusha mashairi yale mazuri. Si tu kitakuwa ni chanzo chako cha kujiburudisha bali inakuza utendaji wa akili yako kukupeleka katika ngazi ya juu zaidi katika kumbukumbu, kuunganisha mambo mbalimbali na wepesi wa akili.
126. Maneno yako yawe laini na hoja zako nzito.
Kwa leo tuishie hapa na karibu tena,
\\ujasiriamaliafya
georgemtega@gmail.com; Whatsap/Telegram (+255 625 843 804)

Hakuna maoni: