Kuna
magonjwa ya matumbo yajulikanayo kitaalam kama Peptic Ulcer (Gastric Ulcer,
Stomach Ulcer, Duodenal Ulcer) au kwa lugha iliyozoeleka kama Vidonda vya
tumbo.
Magonjwa
haya yote kwavile yote ni ya tumboni wapo watu wengi wameteseka nyakati ambazo
Daktari hayupo au wapo mbali na matabibu na hata kupoteza maisha. Mimi ndugu
yako leo naomba tusaidiane ni namna gani utakabili hali hii pasipo
daktari.
DALILI ZA UGONJWA WA
VIDONDA TUMBO.
·
Maumivu
makali yenye dalili za kiungulia dakika 45 - 60 baada ya kula chakula au wakati
wa usiku. Ukinywa maji glasi moja kubwa au ukila chakula utaona kuna kutulia.
Wakati mwingine kutapika na kukudhohofisha mwili. Wakati mwingine yataanza
majira ya saa saba hadi saa nane usiku. Maumivu chini ya kifua yanayoendelea.
Hii ni dalili ya vidonda vya tumbo bila ubishi.Maumivu haya wakati mwingi wengi
husema ni kiungulia au njaa.
·
Dalili
zingine ni kama; Maumivu ya kichwa,kuhisi harufu mbaya, Maumivu chini ya
mgongo, Kuwashwa na au kutapika.
SABABU:
·
Sababu
ya magonjwa haya wataalam wanatuambia ni ulaji chakula usio stahili au ulaji
chakula unaopita kipimo. Wakati mwingine inakuwa ni sababu ya msongo wa mawazo
au maumivu ya neva katika miili yetu.
·
Kuta
za matumbo yetu huzalisha asidi iitwayo inayofanya kazi ya kuyeyesha protein mwilini
mwetu. Licha kuwa kuta zenyewe za matumbo yetu yenyewe yana proteini, asidi
hiyo hainaga madhara kwenye matumbo yetu ingawa chakula tunachokula au matatizo
ya hali ya mtu ndipo shida huanza. Matatizo hayo hupelekea aside hiyo kuyeyusha
kuta za matumbo yetu kwasababu asidi iliyozalishwa imezidi au ute unaolinda
kuta hizo unapokuwa hauzalishwi vilivyo.
·
Vidonda
hivi vya tumbo hutokea kwenye esophagus au umio, lakini kawaida hutokea kwenye
tumbo au utumbo mwembamba. Vidonda vya tumbo hutokea mara 2 ½ zaidi kwa wanaume
zaidi ukilinganisha na wanawake kwenye umri wa miaka 40-55. Vidonda vya tumbo katika
utumbo mwembamba hutokea kwa mara ya kwanza inchi 11 tokea tumboni yaani
stomach nah ii ni kwasababu ya kuzidi hiyo asidi iitwayo HCL. Vidonda tumbo
hivi hutokea zaidi kwa wanaume mara nne zaidi ya wanawake kwenye umri wa miaka
25-40.
·
Huko
Amerika 15% ya watu wake wana vidonda tumbo. Lakini ni nusu yake tuu ndio
hutibiwa. Wengi hugundulika baada ya kuanza kutapika damu. Vitu vinavyochangia
kuzalishwa kwa hiyo asidi HCL mwilini zaidi ya kawaida ni pamoja na wasiwasi
pamoja na msongo wa mawazo. Aspirini, dawa za kuzuia uvimbe na uvutaji sigara
vyote hivi vinaongeza HCL kwenye matumbo.
·
Unaposikia
maumivu ya tumbo kwa dalili nilizoorodhesha hapo juu kunywa juisi ya limao
ukiona hali inazidi basi fahamu HCL imezidi kwenye matumbo. Na kama unatapika
damu au unapata choo chenye damu una hatari ya kuvuja damu hadi kifo unapaswa
kuwahi kuwaona matabibu Hospitalini. Na kama ukinywa juisi ya limao na maumivu
yakatoweka basi fahamu una upungufu wa HCL kwenye matumbo yako.
MATIBABU PASIPO DAKTARI:
·
Kunywa
maji katika glasi kubwa ili kuondosha maumivu kwa haraka.
·
Maji
yanapunguza nguvu ya asidi na kutoa nje asidi hiyo.
CHAKULA:
·
Kula
chakula kidogo siyo mpaka uhisi tumbo limejaa.
·
Viazi
mviringo ni vizuri zaidi.
·
Juisi
ya kabichi ukichanganya na karoti na uinywe mara 4 kwa siku.
·
Kula
mbogamboga kwa wingi.
·
Mchele
mweupe na mtama uliopikwa vizuri pia unafaa.
·
Maziwa
pia si mazuri kwa mgonjwa wa vidonda tumbo maana yanafanya asidi izalishwe
zaidi.
·
Madaktari
wa india wanatumia unga wa ndizi kutibu vidonda tumbo hivyo basi ndizi mbivu ni
nzuri pia.
·
Kula
vyakula vingine vyenye vitamin A, Zinc, Copper, Glutamine kadiri matabibu
watakavyokushauri.
EPUKA:
·
Epuka
mazingira yote yanayokufanya uwe na wasiwasi, msongo wa mawazo, na au uoga.
·
Epuka
vyakula vilivyo na caffeine, uvutaji sigara, na usinywe maziwa ya ng`ombe.
·
Matumizi
ya chumvi yaliyozidi.
·
Chakula
chenye sukari nyingi.
·
Mkate
mweupe yaani white bread.
·
Kula
bila utaratibu.
·
Dawa
za kutuliza maumivu.
MAMBO MENGINE YA KUFANYA:
·
Mazoezi
ya wastani hupunguza msongo wa mawazo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni