Heri
ya Mwaka mpya ndugu yangu na msomaji wa makala zetu za “ujasiriamaliafya”
kwanza napenda kutumia nafasi hii kukupongeza wewe binafsi pamoja na familia
yako yote kwamba hatimaye tumepata kibali kwa yeye aliyetupa pumzi hii kuuona
mwaka 2017. Mungu akubariki sana na
ninakutakia mwendo salama katika njia yako ya mafanikio katika mwaka huu wa
2017. “HAPPY NEW YEAR 2017” na “HERI YA MWAKA MPYA 2017”.
Tofauti
na tulivyozoea leo katika andiko langu nitajaribu kutumia nukuu za Biblia kwani
mimi kwa neema niliyopewa ni mwanafunzi wa Biblia pia. Hata hivyo kwa kuthamini
imani za watu wengine wasiotumia Biblia naomba tuchukuliane hivyo kwani ni
muhimu kufahamu katika uchambuzi wa mambo mbalimbali nukuu kutoka vyanzo
mbalimbali pia zinahitajika sana ili kutufanya tuelewe maarifa haya kuwa si
kitu kipya sana bali ni katika kukumbushana kwa nia ya kutufanya tuende vyema
katika safari yetu ya mafanikio.
Mungu
Muumbaji wetu sisi binadamu anahitaji kuona kila mmoja anafanikiwa na katika
kukamilisha mapenzi hayo kwetu ametutengenezea njia pia kwa kila mmoja kumfanya
afanikiwe.
Mungu
anapenda kila mmoja aishi maisha yenye mahusiano na yeye, yaani tuishi mbali na
masumbufu mbalimbali, tuwe na familia njema, tuwe na kipato kizuri, tuishi na
jamii inayotuzunguka iliyofanikiwa n.k.
Sasa
basi katika kukamilisha hili upo uwekezaji ambao Mungu ameufanya kwa kila mmoja
wetu. Ndani yako kuna uwekezaji uliofanywa na Mungu siku ile ulipoumbwa. Hakuna
mmoja wapo yeyote aliyeumbwa na Mungu akaachwa tupu. Wewe siyo MTUPU uko
uwekezaji uliofanywa na Mungu ndani ya kila mmoja. Uwekezaji huo ni wa vitu
sita vifuatavyo;-
- Maisha: Kila mmoja anazaliwa na anaishi sawa sawa. Tunazaliwa, tunakua hadi tunafikia uzee hatua hizi za maisha kila mmoja anapitia.
- Muda: Katika siku moja tuna masaa 24 na kila mmoja anayatumia masaa hayo hakuna mmoja anayeweza kusema amepewa masaa mengi zaidi au pungufu zaidi ya mwingine wote tuna masaa yanayolingana.
- Kipaji na Uwezo: Kila mmoja ana kipaji au uwezo aliowekewa ndani mwake unaomtofautisha huyu na yule.
- Neema ya Kumuwezesha: Kila mmoja amewekewa kitu ndani yake cha kumfanya atende au afanye jambo ambalo hatimaye atagundua si kwa uwezo wake wala nguvu zake bali upo msaada usioonekana uliomfanikisha jambo lile.
- Ahadi: Zipo ahadi ambazo Mungu ametoa kwa kila mmoja bila upendeleo na uwezekano wa kuzipokea ahadi hizo. Mfano ahadi za uzima, chakula, mavazi, hekima, maarifa, n.k. 3Yohana 1:2 “mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako ....”
- Fursa: Kila siku ni mpya ndiyo maana kuna sekunde, dakika, siku, wiki, miezi, miaka na vyote havifanani kabisa.
Sasa
mgogoro upo kwenye namna kila mmoja anavyoutumia uwekezaji huo. Na matokeo
ndiyo yanatupa majibu ya ni namna gani huyu au yule ametumia uwekezaji uliomo
ndani mwake. Maana majibu ni dhahiri kabisa!!!
Ndugu
yangu fahamu hatujaumbwa na Mungu kama roboti, kama tungeumbwa na Mungu kama
roboti kila jambo lingefanywa nasi kulingana na Mungu alivyoweka programu ndani
mwetu lakini tangu mwanzo anatuonesha kuwa baada ya kutuumba alitupa vitu
vitatu vya kutuongoza katika njia ya mafanikio MWANZO. 2: 15-17;-
- Uhuru wa kuamua: Tumepewa uhuru binafsi wa kuamua ili tutofautishwe na roboti.
- Dhamiri ya kutuongoza: Kila mtu anaye mtu wa ndani asiyeonekana kwa macho ambaye utaisikia sauti yake akikwambia fanya hivi au vile. Hiyo ndiyo dhamiri.
- Uhuru wa Kuchagua: Kila mmoja ana uhuru wa kuchagua; unaweza kuchagua ulale siku nzima au usilale, umchague kiongozi yupi na yupi umuache na hapa ndipo kwenye hatari maana unaweza kumchagua fisi awe kiongozi au sokwe au usichague kabisa.
Upo
jinsi ulivyo kwa kuwa umechagua uwe jinsi ulivyo na nikuhakikikishie hakuna
unayepaswa kumlaumu, kwamba nipo jinsi nilivyo kwasababu ya serikali, au
kwasababu ya wazazi wangu, au kwasababu ya mume wangu, au mke wangu, au watoto
wangu , au walimu wangu, au mchungaji wangu, au shule yangu, au chochote, n.k.
HAPANA umechagua mwenyewe uwe jinsi ulivyo.
Kila
mmoja ana wajibu binafsi wa namna anataka maisha yake yaende. Kumlaumu yeyote
ni kukwepa wajibu wako binafsi. Wewe binafsi unawajibika kwa hayo usiyoyataka.
Mwingine
utasikia anasema Nchi yetu ni masikini, au wilaya yangu ni masikini, au familia
yetu ni masikini; NIKUULIZE SWALI; Je kuna nchi inayozalisha umasikini? Au kuna
wilaya, au familia inayozalisha umasikini? Hii ni kukwepa kuwajibika kwa kila
mmoja binafsi.
Unao
uhuru wa kuchagua umasikini au kuchagua utajiri. Na matokeo ya kuchagua
ulichochagua ndiyo yamekuweka uwe ulivyo.
Mafanikio
hayaji kwa kusoma na kuchagua misingi miwili au mitatu ili kufanya mageuzi ya
maisha yako na nikuhakikishie kwamba kama maisha uliyonayo unayachukia amua
kugeuka kabisa na ubadili uelekeo kama kufanya “engine overhaul” unapangua
vyote usivyovitaka na kuweka unavyovitaka na kuanza safari ya mafanikio
sasa.!!!! Hapa si Mungu wa kukugeuza ni wewe kuamua kufanya “engine overhaul”
ya safari yako ya mafanikio maana hayo ni matokeo ya uhuru wako binafsi.
Ukisema tangu sasa inawezekana mimi kuwa tajiri maana yake umasikini
umeshindwa. Maana upo huru kuwa tajiri au kuwa masikini.
Mafanikio
siyo sehemu Fulani, mafanikio ni safari ndefu tena isiyo na mwisho; huwezi
kufika mahali alafu ukasema sasa nimefanikiwa. Ni safari unayoenda hatua kwa
hatua na ni ndefu sana, haina mwisho.
Katika
safari hii ya mafanikio vipo vitu unavyopaswa kusafiri navyo ili kuifanikisha
safari ya mafanikio;-
Ni
lazima utembee na utayari: katika 1Samweli 16:7 katika mistari hii Mungu
inatwambia Mungu haangalii sura ya nje, anaangalia utayari wako ndani katika
kukufanikisha kwenye safari yako. Sura ya nje inadanganya sana ndugu yangu
Mungu anataka;-
- Moyo wa unyenyekevu kwenye safari hiyo.
- Utayari wa kukubali makosa yako.
- Utayari wa kujifunza.
- Ni lazima utembee na lengo mahususi: Hatupo hapa kwa bahati mbaya, tupo hapa kwa mpango maalum wa Mungu.
- Uushikilie vizuri muda wako uliombele.
- Tengeneza taswira ya maisha yako, unataka maisha ya namna gani?
- Amua unataka ukumbukwe kwa lipi baada ya maisha haya?
Itaendelea
kipindi kijacho.........
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni