Sifa
za banda bora la Kuku
Ukiamua kufuga
katika banda kwa njia mbili zilizoelezwa awali utatakiwa kujenga banda
kama ifuatavyo:
- Pasiwe na sehemu zilizo wazi kwenye msingi na kati ya ukuta na paa.
- Banda lijengwe na vifaa vinavyopatikana katika mazingira yako ili liwe na gharama utakayoweza kumudu.
- Unaweza kutumia matofali ya udongo, udongo, miti, fito,n.k. Ukitumia fito au mabanzi ondoa maganda ili kuthibiti mchwa.
- Jengo imara litazuia maadui kama panya, vicheche, paka, nyoka na wezi kuingia ndani ya banda na kuwadhuru au kuwaiba kuku.
• Kuta na sakafu visiribwe zisiwe na nyufa ili kurahisisha
kusafisha.
• Pia itadhibiti kusiwe na wadudu wa kujificha katika nyufa kama
papasi, viroboto n.k.
urahisi katika mazingira yako.
• Matandazo haya husaidia kunyonya unyevu unaotokana na kinyesi
cha kuku au maji
yanayomwagika katika banda.
• Banda hubakia kavu bila kuwa na harufu mbaya na wadudu kama inzi
hata vimelea
vya magonjwa hudhibitiwa.
Eneo
la nje kuzunguka banda kuwe na usafi wa kudumu
Hali ya usafi
nje ya banda itafanya wadudu kama siafu au mchwa na wanyama kama panya na paka
mwitu wakose maficho. Nje ya banda ndani ya uzio kuwe na miti midogo na mimea mingine midogo kwa ajili
ya kivuli.
Ufugaji
nusu huria
Kwa kawaida
eneo la mita mraba moja hutosha
kuku wanne
wanaotaga au kuku 8 wa nyama.
Nafasi ya mita
mraba 1 inatosha vifaranga 16
hadi kufikia
umri wa majuma manne.
Liweze
kuingiza hewa na mwanga wa
kutosha:
Banda linaloweza kuingiza hewa
safi na kutoka
ndani yake hubaki kavu. Harufu
mbaya hutoka na
kuku huweza kupumua hewa
safi. Hii
husaidia pia kudhibiti kuzaliana kwa
vimelea
vinavyosababisha magonjwa,hivyo
hudhibiti magonjwa.
Lisiwe na
joto sana au baridi sana: Panda miti ya kuzunguka banda lako ili eneo
liwe
na kivuli cha kutosha na
pia lisiwe na upepo mkali.Kama hali halisi ya eneo la kufugia ina
joto kubwa kwa vipindi
virefu paa la banda wakati wa ujenzi liinuliwe juu zaidi kuruhusu
mzunguko zaidi wa hewa na
joto la paa ( kama ni la bati) liwe mbali juu ya kuku.
Joto kwenye banda linaweza
kusababishwa na msongamano wa kuku, hivyo mfugaji
aangalie aweke idadi ya kuku inayowiana na
ukubwa wa banda lake.
Paa
Paa lifunike ukuta kwa sehemu kubwa |
nyasi, madebe, makuti n.k. kutegemeana na
upatikanaji wa vifaa vya
kuezekea.Wakati wa
kuezeka paa lisiishie karibu sana na ukuta bali
kuezeka paa lisiishie karibu sana na ukuta bali
liwe na sehemu kubwa
iliyozidi ukuta kuzuia
mvua kuingia ndani kama ni ya upepo ( angalia
mvua kuingia ndani kama ni ya upepo ( angalia
mchoro hapa chini).
Vifaa
vinavyohitajika katika banda la kuku
Kuku wakifugwa kwa mtindo
wa nusu ndani na nusu nje wanahitaji huduma mbalimbali
ndani ya banda na ndani ya
wigo. Ili kutoa huduma hizi vifaa vifuatavyo ni muhimu viwe
katika banda:
Vyombo vya Maji
Kinywesheo cha kujitengenezea |
Kinywesheo |
• Aina ya mojawapo unayoweza kutumia ndoo au debe
la lita kumi au ishirini ya plastiki. Kata ndoo hiyo pande nne
kutoa nafasi ya kuku ya kunywea
kama kielelezo kinavyoonyesha. Tengeneza idadi ya vyombo hivi inayowiana na
wingi wa kuku ulionao.
• Au waweza kutumia sufuria au beseni pana kiasi.
Hii huwekewa tofali au jiwe safi pana baada ya kuwekewa maji ya kunywa ili kuzuia
kuku wadogo wasizame na maji yasichafi liwe kirahisi.
• Vifaa maalum vya kunyweshea kuku vinapatikana
katika maduka ya pembejeo zakilimo.
Vyombo vya
Chakula
Vyombo hivi ni muhimu viwe
vimetengenezwa vizuri ili visiwe chanzo cha upoteaji wa chakula.
Unapotengeneza kilishio cha
kuku kumbuka kuwa kuku wana tabia ya kuchakura. Husambaza
au kupekua chakula kwa miguu
hata kwa midomo ili kupata chakula cha chini.
Kilishio |
Tabia hii husababisha
kumwagwa kwa chakula kingi chini na kusababisha hasara. Unaweza kudhibiti tatizo
hili kwa kutengeneza vyombo visivyoruhusu kuku kuchakura kama inavyoonyeshwa kwenye
kielelezo hapa chini.
Unaweza kutengeneza
kilishio hiki wewe mwenyewe au fundi seremala waliopo katika eneo unaloishi. Inafaa
kilishio kiwe chembamba ili kuku wasiweze kuingia. Pia kinatakiwa kiwe kirefu ili kuku waweze kula bila kusongamana.
Viota
ya kutagia kuku mmoja
mmoja. Vipimo vinavyopendekezwa kwa kila kiota ni upana wa
sentimita 30, urefu
sentimita 30 na kina sentimita 35. Upande wa mbele uachwe waziila sentimita 10
za kwanza kutoka chini zizibwe na ubao ( angalia kielelezo). Weka idadi ya
viota inayotosheleza
kuku ulio nao.
Muunganiko wa Viota |
Pia ipo aina nyingine
inayoweza kutumiwa na kuku zaidi ya mmoja kwa wakati mmoja. Ni kama kiota
kimoja kilichogawanywa
katika vyumba kadhaa. Ila kila chumba kina vipimo kama vya kiota kimoja(
angalia picha hapa
chini).Aina hii ya kiota ina upana wa sentimita 30 na kina sentimeta 35 na
urefu wake unategemea idadi ya viota.
Viota vinatakiwa kuwa na
giza ili kuku wasiogope kuingia kutaga ndani yake. Pia giza
husaidia kupunguza tabia ya
kuku kula mayai na kudonoana. Kiota kinafaa kuwekwa
mahali ambako ni rahisi
kuku kuingia na kutoka. Vile vile iwe ni sehemu itakayorahisisha
usafishaji wa kiota chenyewe.
Vichanja
Kuku wana asili ya kupenda
kulala au kupumzika sehemu iliyoinuka. Hivyo ndani ya
banda weka vichanja
vitakavyotosheleza idadi ya kuku waliopo.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni