Alhamisi, 22 Septemba 2016

UTANGULIZI KUHUSU UJASIRIAMALI NA AFYA



Mpendwa msomaji na rafiki yangu katika mtandao wetu wa kijamii! Salaam!
Nimeanzisha mtandao huu kwa nia ya kushirikishana mambo mbalimbali yahusuyo Ujasiriamali na Afya kwani baada ya kupitia makala mbalimbali za Waandishi mbalimbali maarufu duniani na wana-falsafa mbali mbali nimegundua hakuna mwanadamu yeyote ambaye amezaliwa ili awe masikini licha ya wengi kudhani kuwa umasikini ni sehemu ya jamii fulani au familia fulani. Blog yangu inaitwa “ujasiriamaliafya” hapa yameunganishwa maneno mawili ujasiriamali na afya. Hii ni kwasababu mjasiliamali yeyote ili kufikia ndoto za mafanikio yake hana budi kuwa na afya njema. Hivyo basi mambo ambayo tutashirikishana hapa ni yale yahusuyo mafanikio na afya zetu.
Kubwa la kufahamu hapa na kulikumbuka ni kwamba “akili yako mwenyewe ndiyo yaweza kukufanya uwe masikini au tajiri” hii ni kwasababu mambo yote yanaanzia kwenye akili. Jinsi unavyojiona na jinsi unavyojisikia na kujitambua ndiyo maisha yako yatakavyokuwa.
Endelea kufuatilia mambo haya kupitia www.ujasiriamaliafya.blogspot.com

Hakuna maoni: